Sunday , 19 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Msajili aikalia kooni TLP nafasi ya Mrema
Habari za SiasaTangulizi

Msajili aikalia kooni TLP nafasi ya Mrema

Agustino Mrema
Spread the love

OFISI ya Msajili wa Vyama vya Siasa, imekitaka Chama cha Tanzania Labpour Party (TLP), kuitisha uchaguzi wa kujaza nafasi ya mwenyekiti wake taifa, iliyoachwa wazi na Augustino Mrema, aliyefariki dunia Agosti 2022. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Agizo hilo limetolewa na ofisi hiyo kupitia barua yake iliyotolewa na  Naibu Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, Sisty Nyahoza, mwishoni mwa Juni mwaka huu, akijibu malalamiko ya baadhi ya wanachama wa TLP kuhusu kusitishwa kwa uchaguzi wa chama hicho zaidi ya mara mbili pasina sababu za msingi.

“Ibara ya 24 ya katiba ya TLP inaeleza kuwa, nafasi ya uongozi ikiwa wazi inapaswa kujazwa mara moja. Hivyo kwa kuwa Mrema alifariki tarehe 21 Agosti 2022 na TLP mlipanga kufanya uchaguzi kujaza nafasi hiyo tarehe 6 Machi 2023 uchaguzi huo haukufanyika  hivyo mnapaswa kuandaa uchaguzi mwingine kujaza nafasi ya mwenyekiti ili ile dhana ya mara moja iliyoelezwa katika katiba yenu itekelezwe,” imesema barua hiyo.

Kupitia barua hiyo, Msajili amemtaka Kaimu Mwenyekiti Taifa TLP, kuitisha mkutano mapema iwezekanavyo ili uchaguzi wa kujaza nafasi hiyo ufanyike haraka iwezekamnavyo.

Hii ni mara ya pili kwa Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, kuiandikia barua TLP ikiitaka uongozi wake ujieleze kwa nini umeshindwa kufanya uchaguzi huo.

Ni baada ya mkutano ulioandaliwa kufanya uchaguzi huo Machi 2023, kuahirishwa kwa madai ya kugubikwa na vitendo vya rushwa baina ya wagombea.

Leo tarehe 10 Julai 2023, MwanaHALISI Online imemtafuta Makamu Mwenyekiti wa TLP, Hamad Mkadamu Rajabu, ili kufahamu utekelezaji wa agizo hilo amesema maandalizi yanafanyika hivyo uchaguzi huo unatarajiwa kufanywa Agosti mwaka huu.

“Hatujapanga siku gani utafanyika lakini tunatarajia mwezi Agosti utafanyika. Tutakaa hivi karibuni na Msajili wa Vyama vya Siasa kasha tutapanga namna ya kutekeleza agizo hilo,” amesema Mkadamu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

CCM yamteua Pele kuwa mgombea ubunge Kwahani

Spread the loveKamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM)...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Ujenzi kituo cha kupoza umeme Chalinze wafikia asilimia 93.7

Spread the loveKamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imeeleza...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Wakili Mwabukusi anusurika kufungiwa, asema hatarudi nyuma

Spread the loveWAKILI Boniface Mwabukusi amesema kuwa hatorudi nyuma kuwatetea Watanzania na...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

RC Chongolo atangaza ‘vita’ kwa wanaovusha wageni kinyemela

Spread the loveKATIKA kulinda usalama wa nchi kupitia mpaka wa Songwe, Mkuu...

error: Content is protected !!