Sunday , 19 May 2024
Home Kitengo Maisha Afya NHIF yaita Watanzania kujisajili uanachama Sabasaba
Afya

NHIF yaita Watanzania kujisajili uanachama Sabasaba

Spread the love

MFUKO wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), umewahimiza wananchi wa mkoa wa Dar es Salaam na waliotoka katika maeneo mbalimbali nchini kufika katika Banda la NHIF katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere ili kupata huduma ya kusajili kuwa wanachama. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Rai hiyo imetolewa leo tarehe 30 Juni 2023 na Meneja Uhusiano wa Mfuko huo, Anjela Mziray ambaye ameeleza kuwa, kupitia Maonesho ya 47 yanayoendelea sasa katika viwanja hivyo, Mfuko unatoa huduma ya usajili wa wanachama kupitia mpango wa Vifurushi ambao unamwezesha kila mwananchi kujiunga na kunufaika kwa kuwa na uhakika wa matibabu.

Amesema kuwa mbali na usajili wa wanachama, Mfuko pia unatumia fursa hiyo kutoa elimu ya dhana ya bima ya afya na umuhimu wa kujiunga kabla ya changamoto za afya, kupokea mrejesho wa huduma na maoni ya uboreshaji wa huduma na kushughulikia changamoto mbalimbali walizokutana nazo wanachama.

“Tuko hapa Sabasaba katika Jengo la NHIF na mwaka huu tumekuja na huduma ya usajili wa wanachama, kuhuisha uanachama, kutoa usajili kwa waajiri na watumishi wao pamoja na elimu ya bima ya afya,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Afya

Kambi ya matibabu ya kibingwa Ruangwa yaacha vilio, DC atoa ombi JAI

Spread the loveMKUU wa Wilaya ya Ruangwa, Hassan Ngoma amefunga rasmi kambi...

AfyaHabari za Siasa

Serikali yatoa kauli wanaolala nje Hospitali ya Muhimbili

Spread the loveSERIKALI imesema inajipanga kushirikiana na sekta binafsi kujenga majengo yatakayosaidia...

Afya

Mbunge ataka huduma Ultrasound itolewe bure kwa wajawazito

Spread the loveMBUNGE wa Viti Maalum, Esther Malleko, ameitaka Serikali kutoa bure...

Afya

Vituo 13 vyasitishiwa mkataba madai kutaka kupiga bilioni 4 za NHIF

Spread the loveVITUO vya kutoa huduma za afya 13, vimesitishiwa mikataba ya...

error: Content is protected !!