Saturday , 4 May 2024
Home Kitengo Michezo Dk. Mkwizu: Afrika tudumishe utamaduni
Michezo

Dk. Mkwizu: Afrika tudumishe utamaduni

Spread the love

 

MWENYEKITI wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa Mkoa wa Kilimanjaro (ALAAT), Dk. Salehe Mkwizu ameshauri nchi za Afrika kudumisha utamaduni wa bara hilo kwa kuwa ndio urithi usiofutika na endelevu. Anaripoti Mwandishi Wetu, Morocco … (endelea).

Mkwizu amesema hayo wakati akihutubia mkutano wa Mameya wa Afrika unaoendelea jijini Rabat nchini Morroco.

Mkutano huo umehudhuriwa  na mameya 54, mabalozi na mawaziri kutoka nchi zote za Afrika ambapo Tanzania imewakilishwa na Mkwizu ambaye ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga.

Dk. Mkwizu alisema hadi sasa Afrika imeshindwa kufanya mambo mengi ya pamoja kama kuanzisha benki yao, fedha moja na mengineyo.

“Tumekuwa na visingizio vingi katika kuanzisha fedha ya pamoja na mengine, je sasa na hili la kushindwa kulinda tamaduni zetu tutamsingizia nani? Ni wajibu wetu kulinda, kudumisha na kuukuza utamaduni wa Kiafrika kwa maisha bora ya vizazi vyetu vijavyo.

Agenda ya utamaduni ni agenda namba nne ya maendeleo katika Taifa lolote hivyo kama Afrika kuanzia agenda ya kwanza mpaka ya tatu zinatusumbua je na hii ya nne ambayo inatuhusu kwa asilimia 100 bila kutegemea mataifa ya magaharibi nayo tutasema kwa nini imetushinda kuheshimu, kulinda na kudumisha utamaduni wetu? Au katika hili tutarudi tuseme watuwezeshe fedha?’’ alihoji.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Ligi mbalimbali za pesa kuendelea leo

Spread the love Ijumaa ya leo ambapo mechi mbalimbali zinaendelea Duniani Meridianbet...

Michezo

Europa na Conference kukupatia pesa ndefu leo

Spread the love  ALHAMISI ya leo tutaenda kushuhudia mitanange ya kukata na...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

Michezo

Usiku wa Ulaya umerejea kibabe kabisa

Spread the love  LIGI ya Mabingwa barani Ulaya imerejea tena na awamu...

error: Content is protected !!