MWENYEKITI wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa Mkoa wa Kilimanjaro (ALAAT), Dk. Salehe Mkwizu ameshauri nchi za Afrika kudumisha utamaduni wa bara hilo kwa kuwa ndio urithi usiofutika na endelevu. Anaripoti Mwandishi Wetu, Morocco … (endelea).
Mkwizu amesema hayo wakati akihutubia mkutano wa Mameya wa Afrika unaoendelea jijini Rabat nchini Morroco.
Mkutano huo umehudhuriwa na mameya 54, mabalozi na mawaziri kutoka nchi zote za Afrika ambapo Tanzania imewakilishwa na Mkwizu ambaye ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga.
Dk. Mkwizu alisema hadi sasa Afrika imeshindwa kufanya mambo mengi ya pamoja kama kuanzisha benki yao, fedha moja na mengineyo.
“Tumekuwa na visingizio vingi katika kuanzisha fedha ya pamoja na mengine, je sasa na hili la kushindwa kulinda tamaduni zetu tutamsingizia nani? Ni wajibu wetu kulinda, kudumisha na kuukuza utamaduni wa Kiafrika kwa maisha bora ya vizazi vyetu vijavyo.
Agenda ya utamaduni ni agenda namba nne ya maendeleo katika Taifa lolote hivyo kama Afrika kuanzia agenda ya kwanza mpaka ya tatu zinatusumbua je na hii ya nne ambayo inatuhusu kwa asilimia 100 bila kutegemea mataifa ya magaharibi nayo tutasema kwa nini imetushinda kuheshimu, kulinda na kudumisha utamaduni wetu? Au katika hili tutarudi tuseme watuwezeshe fedha?’’ alihoji.
Leave a comment