Sunday , 28 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Fisi aliyeua na kujeruhi watu mkoani Lindi auawa na askari wa TAWA
Habari Mchanganyiko

Fisi aliyeua na kujeruhi watu mkoani Lindi auawa na askari wa TAWA

Spread the love

 

MAMLAKA ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA) imefanikiwa kumuua fisi aliyeua watu wawili na kujeruhi watano katika Wilaya ya Lindi Vijijini Mkoani Lindi. Anaripoti Christina Haule, Morogoro … (endelea).

Kamanda wa Uhifadhi wa Kanda ya Kusini Mashariki, Abraham S. Jullu alisema mnamo tarehe 11 Mei, 2023 majira ya Saa kumi na mbili asubuhi Ofisi yake ilipokea simu kutoka kwa Mtendaji wa Kata ya Milola akitoa taarifa kuwa fisi amejeruhi watu watatu (3) katika Kijiji Cha Rutamba, watu wawili (2) Kijiji Cha Ng’apa na kusababisha vifo vya watu wawili (2).

Amewataja waliojeruhiwa na fisi huyo kuwa ni Suleman Mtambo, Hadija Said, Alpha Ibrahimu, Maria Sabuni na mwingine aliyetambulika Kwa jina moja (Steven) ambao wote walipelekwa Hospitali ya Sokoine Mkoani Lindi huku waliofariki walitambulika Kuwa ni Abilahi Pokosoi (50), na Saidi Makolela (75) ambapo fisi huyo aliawa majira ya mchana baada ya kupatikana.

Aidha, Kamanda Jullu amesema taratibu za kuwasaka fisi wengine katika maeneo mbalimbali ikiwemo Milola na Vijiji vya Wilaya ya Ruangwa zinaendelea na kuona namna bora ya kuwahamisha na kuwapeleka maeneo ya hifadhi.

Hata hivyo, TAWA inatoa pole kwa wahanga wa tukio hili na inatoa rai kwa wananchi wote kutoa taarifa mapema pale wanapowaona Wanyamapori Wakali na Waharibifu katika maeneo yao ili kuwawezesha Askari kuchukua hatua za kuwadhibiti mapema kabla hawajasababisha madhara kwa maisha ya watu na mali zao.

Vilevile, wananchi wanasisitizwa kuchukua tahadhari ikiwemo kuepuka kutembea nyakati za alfajiri na usiku, na kutofanya shughuli za kibinadamu kama vile kilimo na ufugaji pembezoni mwa hifadhi na maeneo ya mapito (Shoroba) ya wanyamapori.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wami Ruvu hawana deni la Rais Samia katika kutunza vyanzo vya maji

Spread the love  BODI ya Maji Bonde la Wami Ruvu, imeendelea kuchua...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde aibana kampuni kutimiza masharti ya mkataba

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameitaka Kampuni ya Xin Tai...

Habari Mchanganyiko

Dk. Jafo aipongeza Oryx kumuunga mkono Samia

Spread the loveWAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na...

Habari Mchanganyiko

Mvungi aendesha kikao kazi cha wataalam wa Regrow

Spread the love  MKURUGENZI wa Idara Sera na Mipango Wizara ya Maliasili...

error: Content is protected !!