Sunday , 19 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Dk. Mpango akemea mivutano kati ya mawaziri na watendaji
Habari za Siasa

Dk. Mpango akemea mivutano kati ya mawaziri na watendaji

Makamu wa Rais, Dk. Philip Mpango
Spread the love

 

MAKAMU wa Rais, Daktari Phillip Mpango, amewataka mawaziri kuepuka mivutano kati yao na watendaji wizarani, badala yake washirikiane kuwaletea maendeleo wananchi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Dk. Mpango ametoa agizo hilo leo tarehe 15 Februari 2023, Ikulu jijini Dar es Salaam, katika hafla ya uapisho wa viongozi walioteuliwa na Rais Samia, jana Jumanne.

“Watendaji bado tunaona changamoto katika wizara mbalimbali naamini mtakwenda mliangalie vizuri. Tumezungumza mara kadhaa Rais ameeleza hii mivutano kati ya naibu waziri, waziri na katibu mkuu haina tija. Mkae kama timu moja kwa ajili ya kuwaletea maendeleo Watanzania,” amesema Dk. Mpango.

Miongoni mwa viongozi walioapishwa ni aliyekuwa Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mohamed Mchengerwa, aliyehamishiwa kuwa Waziri wa Maliasili na Utalii.

Balozi Pindi Chana, ameapishwa kuchukua mikoba ya Mchengerwa katika Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo. Awali Balozi Chana alikuwa Waziri wa Maliasili na Utalii.

Dk. Mpango amewataka mawaziri hao kuketi pamoja kwa ajili ya kubadilishana uzoefu wa kazi walizofanya kwenye wizara zao za awali.

“Wizara ya Maliasili ina historia kidogo, ina mafunzo mengi ni kati ya wizara ambazo zimekuwa na mawaziri wengi mojawapo ni hiyo ambayo ni sekta muhimu sana kwa maendeleo ya taifa letu. Mchango wake katika fedha za kigeni na ajira ni kubwa sana , mmepewa dhamana kubwa kuhakikisha inaendelea kukua na kuchangia maendeleo ya nchi yetu,” amesema Dk. Mpango na kuongeza:

“Vilevile sekta hiyo bahati mbaya sana ina vishawishi vingi, nina uhakika Pindi atakudokeza mengi aliyoona kwenye kipindi chake. Nadhani umejiepusha na vishawishi hivyo kama kwenye vitalu na mengineyo.”

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Wakili Mwabukusi anusurika kufungiwa, asema hatarudi nyuma

Spread the loveWAKILI Boniface Mwabukusi amesema kuwa hatorudi nyuma kuwatetea Watanzania na...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

RC Chongolo atangaza ‘vita’ kwa wanaovusha wageni kinyemela

Spread the loveKATIKA kulinda usalama wa nchi kupitia mpaka wa Songwe, Mkuu...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

RUWASA yachongewa, yateketeza mamilioni kwa maji yenye magadi

Spread the loveSAKATA la ukosefu wa maji wilayani Momba mkoani Songwe limezidi...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Lissu akabidhiwa gari lake, aomba msaada wa matengenezo

Spread the loveMakamu Mwenyekiti wa Chadema Bara, Tundu Lissu leo Ijumaa amekabidhiwa...

error: Content is protected !!