Wednesday , 1 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Diwani Athuman ang’olewa Ikulu kabla ya kuapishwa
Habari za SiasaTangulizi

Diwani Athuman ang’olewa Ikulu kabla ya kuapishwa

Aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu Usalama wa Taifa, Diwani Athuman Msuya
Spread the love

 

RAIS Samia Suluhu Hassan, ametengua uteuzi wa Kamishna Diwani Athumani, katika nafasi ya Katibu Mkuu Ikulu, na kumteua Mululi Majula Mahendeka, kushika wadhifa huo. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Taarifa ya uteuzi huo imetolewa leo Alhamisi, tarehe 5 Januari 2023 na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Zuhura Yunus.

Rais Samia amemtumbua Kamishna Diwani, ikiwa zimepita siku mbili tangu amteua tarehe 3 Januari 2023. Awali, alikuwa Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa.

“Rais Samia ametengua uteuzi wa Kamishna Diwani, aliyemteua tarehe 3 Januari 2023. Aidha, Rais Samia amemteua Mululi Majula Mahendeka, kuwa Katibu Mkuu Ikulu. Mahendeka alikuwa Afisa Mwandamizi wa Ofisi ya Rais, Ikulu,” imesema taarifa ya Zuhura.

 

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!