Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Waziri apanda bodaboda kwenda kukagua mradi wa maji
Habari Mchanganyiko

Waziri apanda bodaboda kwenda kukagua mradi wa maji

Spread the love

WAZIRI wa Maji nchini Tanzania, Jumaa Aweso, amelazimika kutumia usafiri wa pikipiki maarufu kama bodaboda ili kuweza kufika kwenye mradi wa maji wa Morong’anya uliopo jimbo la Morogoro Kusini Mashariki mkoani Morogoro. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Aweso akiwa na Mbunge wa jimbo hilo, Hamis Taletale, walitumia njia hiyo ya usafiri kutokana na eneo kilipo chanzo cha mradi huo kutofikaka kwa njia ya gari.

Mradi huo  unaogharimu kiasi cha Sh 23.1 bilioni,  pindi utakapo kamilika utahudumia wananchi zaidi 52,000 kwenye vijiji 19 vilivyopo katika kata 7 za Jimbo la Morogoro Kusini Mashariki.

Mbali na kukagua mradi huo na kuridhika na maendeleo yake, Waziri huyo pia alishiriki zoezi la kupanda miti kwenye chanzo cha maji cha mto Mbezi utakaotumika kama chanzo cha maji kwa mradi huo mkubwa na wakihistoria katika jimbo la Morogoro Kusini Mashariki na Wilaya ya Morogoro

.

Pia ameshiriki kazi ya kuunganisha mabomba na kuyalaza ikiwa ni moja ya juhudi za utekelezaji wa mradi huu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!