Sunday , 19 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Wasira asema mikutano ya hadhara haitoiathiri CCM
Habari za Siasa

Wasira asema mikutano ya hadhara haitoiathiri CCM

Steven Wasira
Spread the love

MWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Stephen Wasira amesema mikutano ya hadhara ikianza kufanyika itakiamsha Chama kilichoko madarakani cha CCM, ili kitimize mambo iliyoahidi kwa wananchi kupitia Ilani yake ya Uchaguzi Mkuu wa 2020.Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Wasira ameyasema hayo leo Alhamisi, katika mkutano wa mtandaoni ulioendeshwa na taasisi ya Watch Tanzania, baada ya kuulizwa iwapo CCM itaathirika na ruksa iliyotolewa na Rais Samia Suluhu Hassan, kwa vyama vya siasa kufanya mikutano ya hadhara.

Wasira aliyekuwa Mbunge wa Bunda kwa tiketi ya CCM, amesema kitendo cha vyama vya siasa vya upinzani kuruhusiwa kufanya mikutano hiyo, hakitaathiri chama chake.

“Sisi tunasema kama wasimamizi wa ilani kuna faida hakuna hasara yoyote sababu ni chama cha siasa tuemaminiwa na tumeshika dola, tunaendesha Serikali lakini kuna ahadi tumewapa Watanzania katika ilani. Kuruhusu mikutano ya hadhara wanatuamsha zaidi tusilale ili tutimize tulichoahidi lakini tukitetee zaidi,” amesema Wasira.

Aidha, Wasira amevitaka vyama vya siasa kufanya siasa za kistaarabu kwa kuwa siasa za fujo ndiyo ilikuwa sababu ya Hayati John Magufuli, kupiga marufuku mikutano ya hadhara.

Katika hatua nyingine, Wasira amesema Rais Samia anatembea katika maneno yake, kwa kufanya vitu ambavyo aliviahidi ikiwemo kukuza demokrasia na kutoa uhuru kwa vyombo vya habari.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Wakili Mwabukusi anusurika kufungiwa, asema hatarudi nyuma

Spread the loveWAKILI Boniface Mwabukusi amesema kuwa hatorudi nyuma kuwatetea Watanzania na...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

RC Chongolo atangaza ‘vita’ kwa wanaovusha wageni kinyemela

Spread the loveKATIKA kulinda usalama wa nchi kupitia mpaka wa Songwe, Mkuu...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

RUWASA yachongewa, yateketeza mamilioni kwa maji yenye magadi

Spread the loveSAKATA la ukosefu wa maji wilayani Momba mkoani Songwe limezidi...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Lissu akabidhiwa gari lake, aomba msaada wa matengenezo

Spread the loveMakamu Mwenyekiti wa Chadema Bara, Tundu Lissu leo Ijumaa amekabidhiwa...

error: Content is protected !!