Wednesday , 1 May 2024
Home Habari Mchanganyiko TAMWA yapigia chapuo mabadiliko sheria ya habari
Habari Mchanganyiko

TAMWA yapigia chapuo mabadiliko sheria ya habari

Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (Tamwa), Rose Reuben
Spread the love

 

CHAMA cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (TAMWA) kimesema mabadiliko ya sheria ya vyombo vya habari yataakisi maendeleo ya tasnia hiyo pamoja na maendeleo ya Taifa kwa ujumla. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Mkurugenzi Mtendaji wa TAMWA, Dk. Rose Reuben ametoa kauli hiyo leo tarehe 29 Novemba, 2022 wakati akichangia mjadala wa mabadiliko ya sheria ya vyombo vya habari ulioendeshwa na Jukwaa la Wahariri nchini TEF.

Amesema kuwa suala la mabadiliko ya sheria ambalo limewashirikisha wadau wote wa habari ni jambo jema.

Ametoa wito kwa wadau wote kutoa mawazo chanya yatakayoleta mabadiliko.

“Pia uwajibikaji wetu kama wadau tunapaswa kutoa mawazo yetu lakini kufika pahali ambapo tunaweza kukubaliana ili kufanya mchakato wa sheria uende haraka iwezekanavyo,” amesema.

Dk. Rose alisema mabadiliko hayo yatawabadilisha waandishi kufanya kazi kwa mujibu wa taaluma lakini pia nchi itapata maendeleo kutokana na kuendelea kwa tasnia hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Oryx gesi yagawa mitungi, majiko 100 kwa waandishi wa habari Dar

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gesi Tanzania imegawa mitungi 100 ya gesi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

Habari Mchanganyiko

TMA yapongezwa kuimarisha ubora na usahihi wa taarifa za Hali ya Hewa

Spread the love  WAFANYAKAZI wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA),...

error: Content is protected !!