Thursday , 18 April 2024
Home Habari Mchanganyiko TAMWA yapigia chapuo mabadiliko sheria ya habari
Habari Mchanganyiko

TAMWA yapigia chapuo mabadiliko sheria ya habari

Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (Tamwa), Rose Reuben
Spread the love

 

CHAMA cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (TAMWA) kimesema mabadiliko ya sheria ya vyombo vya habari yataakisi maendeleo ya tasnia hiyo pamoja na maendeleo ya Taifa kwa ujumla. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Mkurugenzi Mtendaji wa TAMWA, Dk. Rose Reuben ametoa kauli hiyo leo tarehe 29 Novemba, 2022 wakati akichangia mjadala wa mabadiliko ya sheria ya vyombo vya habari ulioendeshwa na Jukwaa la Wahariri nchini TEF.

Amesema kuwa suala la mabadiliko ya sheria ambalo limewashirikisha wadau wote wa habari ni jambo jema.

Ametoa wito kwa wadau wote kutoa mawazo chanya yatakayoleta mabadiliko.

“Pia uwajibikaji wetu kama wadau tunapaswa kutoa mawazo yetu lakini kufika pahali ambapo tunaweza kukubaliana ili kufanya mchakato wa sheria uende haraka iwezekanavyo,” amesema.

Dk. Rose alisema mabadiliko hayo yatawabadilisha waandishi kufanya kazi kwa mujibu wa taaluma lakini pia nchi itapata maendeleo kutokana na kuendelea kwa tasnia hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mume auwa mke kwa kumchoma visu, ajisalimisha Polisi

Spread the loveJACKSON Kalamji (49), anashikiliwa na Jeshi la Polisi jijini Mwanza,...

Habari Mchanganyiko

Serikali yatoa ajira watumishi 46,000, yatangaza utaratibu mpya kuajiri

Spread the loveSERIKALI imetangaza nafasi za ajira za watumishi wa umma 46,000...

Habari Mchanganyiko

Dereva ajali iliyoua wanafunzi Arusha afikishwa kortini, aomba apelekwe rumande

Spread the loveDEREVA aliyehusika katika ajali la basi la Shule ya Msingi...

Habari Mchanganyiko

Dereva ajali iliyoua wanafunzi Arusha afikishwa kortini, aomba apelekwe rumande

Spread the love  DEREVA aliyehusika katika ajali la basi la Shule ya...

error: Content is protected !!