Friday , 17 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mtutura: Wabunge wa CCM wameonewa
Habari za Siasa

Mtutura: Wabunge wa CCM wameonewa

Spread the love

KATIBU wa chama cha ACT-Wazalendo mkoa wa kichama Selou, Abdallah Mtutura amesema kitendo cha CCM kupeleka wabunge wasioweza kuwasema wananchi wao ni kuwaonea wabunge hao. Anaripoti Faki Sosi, Tunduru … (endelea).

“Mtu ukimpa kitu asichoweza kukimudu au kukidhibithi unakuwa umemuonea.”

Kauli hiyo ameitoa leo kwenye ziara ya Katibu Mkuu wa Chama hicho Ado Shaibu kwenye jimbo la Tunduru Kaskazini kata ya Ligula.

Mtutura amesema kuwa asilimia 70 wabunge wa Chama Cha Mapinduzi hawana uwezo wa kuwasemea wananchi bungeni.

Amesema kuwa uchaguzi wa mwaka 2020 haukuwa huru wala wa haki na matokeo yake wakapelekwa watu ambao hawakustahili kuwa wabunge ndio sababu ya kushindwa kuwatetea wananchi bungeni.

Amesema kuwa wabunge hawasemi kama wananchi wanaonewa, tembo wanavamia makazi na mashamba ya watu, hawasemi mgogoro wa wakulima na wafugaji unaoweza kusababisha machafuko.

Mtutura ameongeza kuwa wananchi wamezidiwa na shida hakuna wa kuwasemea. Ametoa wito kwa wananchi kukichagua Chama cha ACT ili wapate sauti mbadala.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari za Siasa

Serikali yatoa kauli wanaolala nje Hospitali ya Muhimbili

Spread the loveSERIKALI imesema inajipanga kushirikiana na sekta binafsi kujenga majengo yatakayosaidia...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Wizara yaomba bajeti ya Sh. 67.9 bilioni, wamachinga watengewa bilioni 10

Spread the loveBAJETI ya Wizara ya maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali yahamasisha uanzishaji vituo vya kulea watoto wachanga

Spread the loveSERIKALI imewahimiza wananchi kujenga vituo vya kulelea watoto wadogo na...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Udhibiti wa serikali wakera asasi za kiraia

Spread the loveBaadhi ya wadau wa demokrasia na viongozi wa asasi za...

error: Content is protected !!