Friday , 17 May 2024
Home Habari Mchanganyiko NMB yaalika wachimbaji wadogo, kati kuchangamkia mikopo ya mitambo
Habari Mchanganyiko

NMB yaalika wachimbaji wadogo, kati kuchangamkia mikopo ya mitambo

Spread the love

KATIKA kuunga mkono juhudi za Serikali za kuwainua wachimbaji wadogo na wa kati kwenye sekta ya madini, Benki ya NMB imetoa wito kwa wachimbaji hao kujitokeza kwa wingi kuchukua mikopo itakayowawezesha kununua mitambo itakayorahisisha shughuli hiyo ya uchimbaji.  Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Wito huo umetolewa leo tarehe 29 Septemba, 2022 na Afisa Uhusiano wa benki hiyo mkoani Geita, Mussa Nyango wakati akimuelezea Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Madini, Msafiri Mbibo kuhusu ushiriki wa NMB katika maonesho ya Kitaifa ya Teknolojia ya Madini yanayofanyika katika viwanja vya Bombambili mkoani Geita.

 

Afisa Uhusiano wa benki ya NMB mkoani Geita, Mussa Nyango (kushoto) wakati akimuelezea Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Madini, Msafiri Mbibo (kulia) kuhusu ushiriki wa NMB katika maonesho ya Kitaifa ya Teknolojia ya Madini yanayofanyika katika viwanja vya Bombambili mkoani Geita.

Nyango amesema katika banda la benki hiyo lililopo katika viwanja hivyo, huduma zote za kibenki zinapatikana ikiwamo kufungua akaunti, huduma ya kuweka na kutoa pesa kwa njia ya wakala na huduma nyingine.

Akizungumzia kuhusu mikopo kwa wachimbaji wadogo, amesema NMB ilijipanga na inaendelea kutoa mikopo kwa wachimbaji hao wadogo, wa kati na wakubwa kwa lengo la kuimarisha shughuli za uchimbaji nchini.

Amesema mikopo hiyo imewawezesha baadhi ya wachimbaji wadogo kukua na kuingia katika kundi la kati kutokana na mitambo ya kisasa waliyoinunua katika shughuli za uchimbaji.

Mbali na wachimbaji hao, amesema benki hiyo inatoa wito pia kwa wajasiriamali wadogo kujiunga na NMB ili kupata mikopo itakayowawezesha kukua kibiashara.

Aidha, akizungumzia jitihada hizo za NMB, Naibu Waziri huyo mbali na kuipongeza benki hiyo, pia alitoa wito kwa wachimbaji wadogo kujitokeza kwa wingi katika maonesho hayo ili kupata fursa ya kufahamu mambo mbalimbali yanayohusiana na kukuza sekta ya madini nchini.

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Madini, Msafiri Mbibo akisaini kitabu cha wageni katika banda la NMB

Maonyesho hayo yanayofanyika kila mwaka, kwa mwaka huu yameshirikisha washiriki zaidi ya 600 wakiwemo 12 kutoka nchi mbalimbali ambao wanaonyesha teknolojia ya uchimbaji wa madini.

Maonyesho hayo ya tano ya kitaifa ya teknolojia ya madini kwa mwaka huu yamebeba kauli mbiu ya “Madini na fursa za uchumi ajira kwa maendeleo endelevu”.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Wizara yaomba bajeti ya Sh. 67.9 bilioni, wamachinga watengewa bilioni 10

Spread the loveBAJETI ya Wizara ya maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na...

Habari MchanganyikoTangulizi

Migogoro ya ndoa yaongezeka, Serikali yawaangukia viongozi wa dini

Spread the loveMIGOGORO ya ndoa na familia imeongezeka kwa asilimia 8.3  kutoka...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali yahamasisha uanzishaji vituo vya kulea watoto wachanga

Spread the loveSERIKALI imewahimiza wananchi kujenga vituo vya kulelea watoto wadogo na...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Udhibiti wa serikali wakera asasi za kiraia

Spread the loveBaadhi ya wadau wa demokrasia na viongozi wa asasi za...

error: Content is protected !!