Wednesday , 22 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Tume ya Madini yataka wachimbaji wadogo kuzingatia sheria ya Mazingira
Habari Mchanganyiko

Tume ya Madini yataka wachimbaji wadogo kuzingatia sheria ya Mazingira

Spread the love

TUME ya Madini imewataka wachimbaji wadogo wa madini ya dhahabu mkoani Geita kuzingatia sheria ya mazingira na afya migodini.

Pia imetoa wito kwa watu wote wanaowekeza katika sekta ya madini wajikinge na walinde mazingira kwenye maeneo wanakochimba Madini hayo. Anaripoti Paul Kayanda, Geita… (endelea).

Hatua hiyo ni kujikinga na vihatarishi vinavyowazunguka katika maeneo yao ya kazi ili wachimbe katika hali ya usalama zaidi na kufaidi kile wanachokipata.

Meneja Habari na Mawasiliano Tume ya Madini, Greyson Mwase akiteta jambo.

Hayo yameelezwa leo tarehe 29 Septemba, 2022 na Afisa mazingira kutoka Tume ya Madini, Hyasinta Laurean katika maonesho ya tano ya kitaifa ya Teknolojia ya Madini 2022 yanayoendelea katika viwanja vya Bombambili mkoani hapa.

“Tupo hapa kutoa elimu kwa Watanzania ili wajue Tume ya Madini inafanya nini, kwa upande wangu naweza kuelezea machache juu ya mazingira na Afya Migodini nawaelezea Watanzania wanaowekeza katika Madini,” amesema Laurean na kuongeza.

“Wanatakiwa wajikinge na walinde mazingira yao yaliyowazunguka na maeneo wanayoyachimba madini hayo kwa mfano kama hapa tuna vifaa vya kujikinga wachimbaji pale wanapokuwa wanachimba ama wanapokuwa wanachenjua dhahabu ili kujizuia na vihatarishi vilivyopo katika maeneo yao ya kazi,” amesema.

Afisa mazingira wa Tume ya Madini, Hyasinta Laurean akifafanua jambo kwa mwandishi wa Habari.

Aidha, Afisa huyo amewataka kuchimba katika hali ya usalama katika maeneo yao ya uchimbaji hatua ambayo watanufaika na kile watakachokipata kwenye shughuli hiyo vile vile kuwalinda na kuwanufaisha watanzania wenzake ambao wapo pembeni.

Kwa upande wake Meneja Habari na Mawasiliano Tume ya Madini, Greyson Mwase ametumia nafasi hiyo kutoa wito kwa wakazi wa Mkoa wa Geita pamoja na Mikoa jirani ya Mwanza, Shinyanga na Kagera kufika kwenye maonesho hayo na kutembelea banda la Tume ili kupata huduma mbalimbali.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Hukumu mahakama kuu yabatilishwa kesi State Oil, Equity Bank Tz

Spread the loveMAHAKAMA ya Rufani, jijini Dar es Salaam, imebatilisha hukumu iliyotolewa...

Habari Mchanganyiko

Geita, Mwanza waongoza kwa mbwa

Spread the loveNaibu waziri wa Mifugo na Uvuvi, Alexander Mnyeti amesema taarifa...

Habari Mchanganyiko

Waziri aipongeza NBS kwa mafanikio

Spread the love  Naibu Waziri wa Fedha, Hamad Chande amepongeza Ofisi ya...

Habari Mchanganyiko

Balozi Nchimbi aonya maofisa utumishi kuacha uonevu

Spread the love  KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dk....

error: Content is protected !!