Saturday , 4 May 2024
Home Habari Mchanganyiko 167 mbaroni kwa tuhuma za kuvunja nyumba, kuiba
Habari Mchanganyiko

167 mbaroni kwa tuhuma za kuvunja nyumba, kuiba

Spread the love

 

JESHI la Polisi nchini, limewakamata watu 167 kwa tuhuma mbalimbali, ikiwemo kuvunja nyumba za raia, kujeruhi na kuiba mali. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Taarifa hiyo imetolewa Leo Jumamosi, tarehe 24 Septemba 2022, jijini Dar es Salaam na Kamishna wa Operesheni na Mafunzo wa Jeshi la Polisi nchini, CP Awadhi Juma, akielezea matokeo ya operesheni maalum iliyofanywa na Polisi kuwakamata watu wanaojihusisha na vitendo hivyo vya kihalifu muda wa usiku wa manane, kwa kutumia silaha za jadi.

Amesema, kati ya watuhumiwa hao, wapo waliokamatwa kwa kosa la kununua mali zinazoibwa na vikundi vya kihalifu maarufu kama panya road.

CP Haji amesema watuhumiwa hao wamekamatwa katika nyakati tofauti Septemba 2022.

“Watuhumiwa hao wamegawanyika katika makundi, kundi la watuhumiwa wanaoshiriki moja kwa moja kuvunja nyumba, uporaji na kundi jingine linalopokea na kununua Mali hizo za wizi,” amesema CP Haji.

Aidha, CP Haji amesema watuhumiwa hao wamekamatwa wakiwa na mali mbalimbali za wizi, ikiwemo runinga za kisasa ‘Flat Tv’, redio na kompyuta.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

RPC Dodoma akabidhiwa bunduki mbili za wahalifu

Spread the love  Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa ya Kulevya...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yazindua huduma maalum kwa wastaafu

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imezindua huduma maalum kwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yazindua akaunti ya Kikundi

Spread the loveBenki ya NMB imezindua akaunti ya kikundi yenye  maboresho makubwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyakazi waidai STAMICO mishahara ya bilioni 1

Spread the loveWALIOKUWA wafanyakazi wa mgodi wa Shirika la Madini la Taifa...

error: Content is protected !!