Tuesday , 23 April 2024
Home Habari Mchanganyiko 167 mbaroni kwa tuhuma za kuvunja nyumba, kuiba
Habari Mchanganyiko

167 mbaroni kwa tuhuma za kuvunja nyumba, kuiba

Spread the love

 

JESHI la Polisi nchini, limewakamata watu 167 kwa tuhuma mbalimbali, ikiwemo kuvunja nyumba za raia, kujeruhi na kuiba mali. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Taarifa hiyo imetolewa Leo Jumamosi, tarehe 24 Septemba 2022, jijini Dar es Salaam na Kamishna wa Operesheni na Mafunzo wa Jeshi la Polisi nchini, CP Awadhi Juma, akielezea matokeo ya operesheni maalum iliyofanywa na Polisi kuwakamata watu wanaojihusisha na vitendo hivyo vya kihalifu muda wa usiku wa manane, kwa kutumia silaha za jadi.

Amesema, kati ya watuhumiwa hao, wapo waliokamatwa kwa kosa la kununua mali zinazoibwa na vikundi vya kihalifu maarufu kama panya road.

CP Haji amesema watuhumiwa hao wamekamatwa katika nyakati tofauti Septemba 2022.

“Watuhumiwa hao wamegawanyika katika makundi, kundi la watuhumiwa wanaoshiriki moja kwa moja kuvunja nyumba, uporaji na kundi jingine linalopokea na kununua Mali hizo za wizi,” amesema CP Haji.

Aidha, CP Haji amesema watuhumiwa hao wamekamatwa wakiwa na mali mbalimbali za wizi, ikiwemo runinga za kisasa ‘Flat Tv’, redio na kompyuta.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

NMB yadhamini Mkutano Mkuu ALAT, kufunguliwa na Samia

Spread the loveBENKI ya NMB, imekabidhi hundi yenye thamani ya Sh. 120...

Habari Mchanganyiko

DC ampongeza Dk. Rose Rwakatare kwa kusaidia waathirika wa mafuriko Mlimba

Spread the loveMWENYEKITI wa Wazazi CCM Mkoa wa Morogoro, Dk.  Rose Rwakatare...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mipango na uwekezaji kutumia bilioni 121.3, mradi wa Bagamoyo wapewa kipaumbele

Spread the loveWIZARA ya Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, imeliomba Bunge...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mbunge ataka kasi uzalishaji walimu ipunguzwe akidai hakuna ajira

Spread the loveMBUNGE wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, ameishauri Serikali ipunguze kasi...

error: Content is protected !!