Friday , 3 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Wananchi wampa tano Samia uboreshaji huduma za kijamii
Habari Mchanganyiko

Wananchi wampa tano Samia uboreshaji huduma za kijamii

Rais Samia Suluhu Hassan
Spread the love

 

MATOKEO ya utafiti uliofanywa na Taasisi ya TWAWEZA kati ya tarehe 18 Juni na 12 Julai 2022 kwa wahojiwa 3,000 waliopigiwa simu, yameonesha asilimia 68 ya wananchi wamefurahishwa na maboresho ya huduma za jamii katika kipindi cha miezi sita iliyopita, hasa sekta ya elimu. Anaripoti Felister Mwaipeta, TUDARCo … (endelea).

Matokeo ya utafiti huo yaliyotolewa leo tarehe 25 Agosti, 2022 pia asilimia 60 wamesema uhuru wa kujieleza umeboreshwa, asilimia 56 wamesema uhuru wa kisiasa umeimarika, asilimia 59 wamesema ulinzi na usalama na kupungua kwa unyanyasaji dhidi ya wanawake (61%) na watoto (60%).

Hata hivyo, asilimia 68 ya wananchi wamesema gharama za maisha zimepanda zaidi katika kipindi hicho, na 48 wamesema upatikanaji wa ajira na fursa za kujipatia riziki za maisha vimepungua badala ya kuongezeka.

“Kwa ujumla, wananchi wengi wanasema nchi iko kwenye mwelekeo sahihi (30%) wachache wanasema nchi haiko kwenye mwelekeo sahihi (25%), ingawa wengi zaidi (44%) wana hali ya sintofahamu kuhusu mwelekeo wa nchi. Matumaini ya wananchi kuhusu suala la uchumi yako chini sana. Idadi ya wanaosema hali ya uchumi ni mbaya ni mara nne (41%) ya wale wanaosema uchumi ni mzuri (9%),” imesema ripoti hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

RPC Dodoma akabidhiwa bunduki mbili za wahalifu

Spread the love  Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa ya Kulevya...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yazindua huduma maalum kwa wastaafu

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imezindua huduma maalum kwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yazindua akaunti ya Kikundi

Spread the loveBenki ya NMB imezindua akaunti ya kikundi yenye  maboresho makubwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyakazi waidai STAMICO mishahara ya bilioni 1

Spread the loveWALIOKUWA wafanyakazi wa mgodi wa Shirika la Madini la Taifa...

error: Content is protected !!