Wednesday , 8 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Heche: Serikali imeshindwa, iwaachie wanaoweza
Habari za SiasaTangulizi

Heche: Serikali imeshindwa, iwaachie wanaoweza

Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, John Heche
Spread the love

 

MJUMBE wa Kamati Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Tanzania, John Heche amesema Serikali iiliyopo madarakani imeshindwa kutatua changamoto za wananchi hivyo “inapaswa kuondoka madarakani na kuwaachia wanaoweza.” Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Heche ameyasema hayo leo Alhamisi tarehe 14, Julai, 2022, akizungumza na waandishi wa habari kuhusu masuala mbalimbali yanayoendelea nchini.

Kada huyo wa Chadema ambaye amewahi kuwa mbunge wa Tarime Vijiji, amesema wajibu namba moja wa Serikali yeyote duniani ni kukusanya kodi kutoka kwa umma na kupeleka huduma,“na wakati wote kuhakikisha wananchi wanatoka kwenye hali ngumu ya kimaisha kwenda kwenye unafuu wa kimaisha.”

Heche amesema “kwa bahati mbaya sana” sehemu kubwa ya Afrika Serikali zinatumikisha wananchi badala ya kuwatumikia na kwamba inatokana na viongozi “kuwa vibaraka, kushindwa kusimamia majukumu yao na kushindwa kusimamiwa vizuri na Mabunge na Mahakama.”

“Na sisi wajibu wetu ni kukumbusha wananchi kwamba kama wamechagua mtu anapaswa kuwatumikia wao kwanza kwasababu bila wananchi hakuna nchi kwasababu wao wamewekwa na watu,” amesema Heche.

Heche amesema nchi “ni kichekesho” kwamba nchi ambayo vijana wake hawana ajira, asilimia 90 ya ngano inayotumia inaagizwa kutoka nje.

“Watu waliopo Serikali ni watu walioshindwa Serikali yenyewe imeshindwa inatakiwa kutoka madarakani iwaachie watu wanaoweza kushughulikia matatizo ya watu,” amesema.

Katika mkutano huo Heche ameeleza namna Serikali inavyochangia kupanda kwa bei ya nishati ya mafuta kutokana na tozo na kodi zilizowekwa.

Amesema licha ya ukweli kwamba bei hiyo imethiriwa na Uviko-19 na vita ya Ukraine na Urusi lakini kwa kiasi kikubwa ni tozo na kodi za Serikali.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Samia: Kuanzia Agosti marufuku kutumia mkaa, kuni

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amemuagiza Waziri wa Nchi, Ofisi ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mwendokasi Kigogo – Segerea kujengwa awamu ya 5

Spread the loveNaibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (TAMISEMI), Festo Dugange...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Rais Samia ni Mzanzibari: Shida Iko Wapi?

Spread the loveTAIFA linakabiliwa na upungufu wa fikra sahihi. Upungufu huu unaonekana...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Mpina mwiba CCM, ahofia kuzibwa mdomo

Spread the loveWAKATI Chama cha Mapinduzi (CCM), kikijinasibu kuwa kinara wa demokrasia...

error: Content is protected !!