Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Heche: Serikali imeshindwa, iwaachie wanaoweza
Habari za SiasaTangulizi

Heche: Serikali imeshindwa, iwaachie wanaoweza

Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, John Heche
Spread the love

 

MJUMBE wa Kamati Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Tanzania, John Heche amesema Serikali iiliyopo madarakani imeshindwa kutatua changamoto za wananchi hivyo “inapaswa kuondoka madarakani na kuwaachia wanaoweza.” Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Heche ameyasema hayo leo Alhamisi tarehe 14, Julai, 2022, akizungumza na waandishi wa habari kuhusu masuala mbalimbali yanayoendelea nchini.

Kada huyo wa Chadema ambaye amewahi kuwa mbunge wa Tarime Vijiji, amesema wajibu namba moja wa Serikali yeyote duniani ni kukusanya kodi kutoka kwa umma na kupeleka huduma,“na wakati wote kuhakikisha wananchi wanatoka kwenye hali ngumu ya kimaisha kwenda kwenye unafuu wa kimaisha.”

Heche amesema “kwa bahati mbaya sana” sehemu kubwa ya Afrika Serikali zinatumikisha wananchi badala ya kuwatumikia na kwamba inatokana na viongozi “kuwa vibaraka, kushindwa kusimamia majukumu yao na kushindwa kusimamiwa vizuri na Mabunge na Mahakama.”

“Na sisi wajibu wetu ni kukumbusha wananchi kwamba kama wamechagua mtu anapaswa kuwatumikia wao kwanza kwasababu bila wananchi hakuna nchi kwasababu wao wamewekwa na watu,” amesema Heche.

Heche amesema nchi “ni kichekesho” kwamba nchi ambayo vijana wake hawana ajira, asilimia 90 ya ngano inayotumia inaagizwa kutoka nje.

“Watu waliopo Serikali ni watu walioshindwa Serikali yenyewe imeshindwa inatakiwa kutoka madarakani iwaachie watu wanaoweza kushughulikia matatizo ya watu,” amesema.

Katika mkutano huo Heche ameeleza namna Serikali inavyochangia kupanda kwa bei ya nishati ya mafuta kutokana na tozo na kodi zilizowekwa.

Amesema licha ya ukweli kwamba bei hiyo imethiriwa na Uviko-19 na vita ya Ukraine na Urusi lakini kwa kiasi kikubwa ni tozo na kodi za Serikali.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!