Friday , 3 May 2024
Home Kitengo Maisha Afya Tozo za miamala ya simu zajenga vituo vya afya 13 Dar
Afya

Tozo za miamala ya simu zajenga vituo vya afya 13 Dar

Aliyekuwa Mkuu wa mkoa wa Mwanza, Amos Makala
Spread the love

 

MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Amos Makalla, amesema fedha kiasi cha Sh. 4.5 bilioni, zilizotokana na tozo za miamala ya simu, zimejenga vituo vya afya 13 mkoani humo. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Makalla ametoa kauli hiyo leo Jumanne, tarehe 5 Julai 2022, mbele ya Rais Samia Suluhu Hassan, katika ufunguzi wa jengo la huduma ya afya ya mama na mtoto katika Hospitali ya CCBRT.

“Napenda kukupongeza (Rais Samia), kwa kazi kubwa uliyofanya kutoa fedha kwa ajili ya kuboresha sekta ya afya kwa mkoa wetu wa Dar es Salaam. Nikushukuru kwa kutoa fedha Sh. 4.5 bilioni, kwa ajili ya vituo vya afya,”amesema Makalla na kuongeza:

“Fedha hizi bilioni 4.5 kwa ajili ya vituo vya afya 13, ni hela za tozo za miamala ambayo sasa tumeanza kuona umuhimu wake. Tozo za miamala tumejenga vituo 13. Tukushukuru pia kwa kuboresha afya umetoa Sh. 14 bilioni, kwenye fedha za UVIKO-19, kuboresha vituo vya afya na hospitali za Dar es Salaam.”

Tozo hizo za miamala ya simu, zilianza kutozwa Julai Mosi, 2021.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari Mchanganyiko

200 wapimwa afya na GGML katika maonesho ya OSHA

Spread the loveZAIDI ya watu 200 jijini Arusha wamejitokeza kupimwa afya na...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

AfyaHabari Mchanganyiko

Songwe katika mikakati ya elimu ya lishe kudhibiti udumavu

Spread the love  SERIKALI mkoani Songwe imejipanga kuendelea kutoa elimu ya lishe...

Afya

Mloganzila yajipanga kupandikizaji wa ini

Spread the love  HOSPITALI ya Taifa Muhimbili-Mloganzila imesema kutokana na uwekezaji uliofanywa...

error: Content is protected !!