Saturday , 20 April 2024
Home Kitengo Maisha Afya Tozo za miamala ya simu zajenga vituo vya afya 13 Dar
Afya

Tozo za miamala ya simu zajenga vituo vya afya 13 Dar

Aliyekuwa Mkuu wa mkoa wa Mwanza, Amos Makala
Spread the love

 

MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Amos Makalla, amesema fedha kiasi cha Sh. 4.5 bilioni, zilizotokana na tozo za miamala ya simu, zimejenga vituo vya afya 13 mkoani humo. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Makalla ametoa kauli hiyo leo Jumanne, tarehe 5 Julai 2022, mbele ya Rais Samia Suluhu Hassan, katika ufunguzi wa jengo la huduma ya afya ya mama na mtoto katika Hospitali ya CCBRT.

“Napenda kukupongeza (Rais Samia), kwa kazi kubwa uliyofanya kutoa fedha kwa ajili ya kuboresha sekta ya afya kwa mkoa wetu wa Dar es Salaam. Nikushukuru kwa kutoa fedha Sh. 4.5 bilioni, kwa ajili ya vituo vya afya,”amesema Makalla na kuongeza:

“Fedha hizi bilioni 4.5 kwa ajili ya vituo vya afya 13, ni hela za tozo za miamala ambayo sasa tumeanza kuona umuhimu wake. Tozo za miamala tumejenga vituo 13. Tukushukuru pia kwa kuboresha afya umetoa Sh. 14 bilioni, kwenye fedha za UVIKO-19, kuboresha vituo vya afya na hospitali za Dar es Salaam.”

Tozo hizo za miamala ya simu, zilianza kutozwa Julai Mosi, 2021.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari za Siasa

Serikali yasaka watumishi afya ngazi ya jamii 8,900

Spread the loveSERIKALI imeanza utekelezaji wa mpango jumuishi wa wahudumu wa afya...

AfyaHabari za SiasaTangulizi

Bima ya afya kwa wote kuanza Aprili, wajane kicheko

Spread the loveSHERIA ya Bima ya Afya kwa Wote, inatarajiwa kuanza kutumika...

AfyaHabari Mchanganyiko

Marekani kuipa Tanzania bilioni 980 kudhibiti VVU, UKIMWI

Spread the loveSERIKALI ya Tanzania inatarajiwa kupewa msaada wa fedha kiasi cha...

AfyaHabari Mchanganyiko

Wanavijiji wajenga zahanati kukwepa umbali mrefu kupata huduma

Spread the loveWANAVIJIJI wa Kata ya  Musanja Jimbo la Musoma Vijijini, mkoani...

error: Content is protected !!