Sunday , 28 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mbunge ataka wananchi waunganishiwe umeme bure
Habari Mchanganyiko

Mbunge ataka wananchi waunganishiwe umeme bure

Mafundi Umeme wakiwa kazini
Spread the love

 

MBUNGE wa jimbo la Mlimba mkoani Morogoro nchini Tanzania, Godwin Kunambi, ameitaka Serikali kuja na mpango wa kuunganisha umeme bure na kisha kukata gharama hizo kidogo kidogo kwenye bili ya mteja. Anaripoti Mwandishi Wetu, Morogoro … (endelea).

Mbunge huyo amesema hilo limekuwa likifanyika katika kuunganisha huduma zingine hivyo linawezekana pia katika sektaya nishati ya umeme.

Kunambi ameyasema hayo leo Alhamisi tarehe 2 Juni, 2022, bungeni jijini Dodoma akichangia hoja hotuba ya bajeti ya Wizara ya Nishati kwa mwaka 2022/23.

“Kwanini Serikali isije na mpango wa wananchi kuunganishwa bure na kisha kutozwa gharama za kuunganishiwa kwenye bili ya umeme kama ambavyo inafanyika katika huduma zingine?” amehoji Kunambi.

Amesema hatua hiyo itarahisisha zoezi la kuunganishiwa umeme “na wananchi wataona unafuu kwamba anaunganishiwa umeme bila gharama.”

“Kaka yangu (Januari Makamba) najua wewe ni fresh minded na una fikra nzuri nikuombe jambo hili ukilifanya utapata credit na serikali itaongeza mapato.”

Katika hatua nyingine Kunambi ameshauri ununuzi wa LUKU uwe wa moja kwa moja kama ilivyo katika ununuzi wa vifurushi vya ving’amuzi.

January Makamba, Waziri wa Nishati

Amesema hiyo itasaidia mtu kuingiza umeme katika mita kupitia simu yake akiwa sehemu yeyote nchini bila kulazimika kwenda kuingiza namba za tokeni kwenye mita.

Akizungumzia mradi wa REA amesema jimboni kwake unatekelezwa kwenye vijiji 11 lakini kuna changamoto wa mkandarasi kutoanza kazi mapema.

“Hata mashimo hajachimba na hata nguzo hajaleta wasiwasi wangu mmesema mradi utakamilika Desemba lakini mkandarasi anaweza kuja kuomba extension ya muda,” amesema Kunambi.

Kuhusu utafiti wa mafuta na gesi Kunambi amesema Tanzania ina uwezo wa kuwekeza na kwamba changamoto sio fedha bali ni uzalendo, mtazamo na uwajibikaji.

“Jambo hili linawezekana nchi yetu ni Tajiri hatuna changamoto ya fedha changamoto kubwa ni uzalendo na mindset na uwajibikaji,”

“Uwezo wako naujua na naibu wako na naamini mna katika hili mna nafasi badoo kwa kutumia mambo haya matatu tunaamini mtakwenda kufanya mambo makubwa sana,” amesema Kunambi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NBC yapata tuzo ya mwezeshaji bora wa mikopo serikali Afrika

Spread the loveBenki ya NBC imepata tuzo ya Mwezeshaji Bora wa Pamoja...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Biteko aipongeza GGML kudhibiti vifo, majeruhi mahali pa kazi

Spread the loveNAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari Mchanganyiko

Wami Ruvu hawana deni la Rais Samia katika kutunza vyanzo vya maji

Spread the love  BODI ya Maji Bonde la Wami Ruvu, imeendelea kuchua...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde aibana kampuni kutimiza masharti ya mkataba

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameitaka Kampuni ya Xin Tai...

error: Content is protected !!