Tuesday , 23 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Chongolo ampe maagizo mbunge wake
Habari za Siasa

Chongolo ampe maagizo mbunge wake

mazao la Alizeti
Spread the love

 

KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Daniel Chongolo amemtaka Mbunge wa Itilima, Njelu Silanga kuwawezesha wakulima wa jimbo hilo kuhakikisha kila tarafa wanapata mashine ya kukamua mafuta ya alizeti. Anaripoti Mwandishi Wetu, Simiyu … (endelea).

Lengo ni kuongeza thamani ya zao hilo ambalo kwa Mkoa wa Simiyu, Itilima inaongoza kwa uzalishaji wa alizeti

“Najua Mbunge wenu ana wajibu wa kuwasaidia mashine za kuchuja mafuta ya alizeti, wasaidie wananchi hawa wapate mashine za kuchuja mafuta ya alizeti angalau kwa mashine moja kwa kila tarafa na hili litawasaidia sana kuongeza thamani ya zao hili.”

Chongolo ametoa maagizo hayo kwa Silanga leo Alhamisi tarehe 2 Juni 2022, alipowasili Wilayani Itilima Mkoa wa Simiyu wakati akiendelea na ziara yake yenye lengo la kukahamasisha uhai wa chama ngazi za mashina na kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

Katibu mkuu huyo alisema kitendo cha kufunga mashine, wakulima wataanza kuuza mafuta badala ya kuuza alizeti zenyewe, ambapo kwa sasa mafuta ya alizeti ndio mafuta bora na ghali zaidi, hivyo wananchi watapata fedha za kutosha tofauti na sasa.

1 Comment

  • Katibu mkuu anatoa maagizo kwa mbunge? Kwani mbunge anawajibika kwa KM? Makubwa haya

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

Habari za Siasa

Serikali kuanzisha mradi wa Gridi ya maji ya Taifa

Spread the loveWaziri wa Maji, Jumaa Aweso amesema katika mwaka wa fedha...

Habari za Siasa

Rais Samia aridhishwa utendaji mabalozi, awapa neno

Spread the loveRais wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan amewapongeza mabalozi  wanaowakilisha ...

error: Content is protected !!