Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Waliolipia 27,000 kabla ya mabadiliko ya bei kuunganishiwa umeme
Habari za Siasa

Waliolipia 27,000 kabla ya mabadiliko ya bei kuunganishiwa umeme

Naibu Waziri wa Nishati, Stephen Byabato
Spread the love

SERIKALI ya Tanzania imesema imetoa maelekezo kwa mameneja wote wa mikoa na wilaya kuwaunganishia umeme wale wote waliokuwa wameshalipia Sh 27,000 kabla ya mabadiliko ya bei. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Hayo yamebainishwa leo Alhamisi tarehe 19 Mei 2022 na Naibu Waziri wa Nishati Stephen Byabato wakati wa kipindi cha maswali na majibu bungeni jijini Dodoma.

Serikali ya awamu ya sita ilibadilisha bei ya kuunganisha umeme katika maeneo ya pembezoni mwa miji kutoka Sh 27,000 za awali na sasa itategemea na umbali wa kutoka kwenye nguzo. Hivi sasa bei hiyo imebakia kwa maeneop ambayo yapo katika vijiji kiutawala.

“Naomba niweke wazi hili kwamba wale wote waliokuwa wamelipia Sh 27,000 kabla ya mabadiliko ya bei waunganishiwe umeme kwa bei hiyo na maelekezo yameshatolewa kwa mameneja wa mikoa na wilaya,” amesema.

Amewataka kuzingatia kuunganisha wale walioanza kupeleka maombi na wateja ambao wamekaa muda mrefu bila kuunganishiwa wawasiliane na Serikali ili kuona tatizo lilipo.

1 Comment

  • Asante ndugu lakini uwelewe badhi inafika mwaka hatujaunganishiwa umeme na tumelipia

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za SiasaTangulizi

Samia awataka watanzania kudumisha muungano

Spread the loveRais wa Tanzania,Samia Suluhu Hassan amewataka Watanzania kuendeleza Muungano kwa...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

error: Content is protected !!