SERIKALI ya Tanzania imesema imetoa maelekezo kwa mameneja wote wa mikoa na wilaya kuwaunganishia umeme wale wote waliokuwa wameshalipia Sh 27,000 kabla ya mabadiliko ya bei. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).
Hayo yamebainishwa leo Alhamisi tarehe 19 Mei 2022 na Naibu Waziri wa Nishati Stephen Byabato wakati wa kipindi cha maswali na majibu bungeni jijini Dodoma.
Serikali ya awamu ya sita ilibadilisha bei ya kuunganisha umeme katika maeneo ya pembezoni mwa miji kutoka Sh 27,000 za awali na sasa itategemea na umbali wa kutoka kwenye nguzo. Hivi sasa bei hiyo imebakia kwa maeneop ambayo yapo katika vijiji kiutawala.
“Naomba niweke wazi hili kwamba wale wote waliokuwa wamelipia Sh 27,000 kabla ya mabadiliko ya bei waunganishiwe umeme kwa bei hiyo na maelekezo yameshatolewa kwa mameneja wa mikoa na wilaya,” amesema.
Amewataka kuzingatia kuunganisha wale walioanza kupeleka maombi na wateja ambao wamekaa muda mrefu bila kuunganishiwa wawasiliane na Serikali ili kuona tatizo lilipo.
Asante ndugu lakini uwelewe badhi inafika mwaka hatujaunganishiwa umeme na tumelipia