Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia asema anazielewa sababu Chadema kususia
Habari za Siasa

Rais Samia asema anazielewa sababu Chadema kususia

Rais Samia Suluhu Hassan
Spread the love

RAIS Samia Suluhu Hassan amesema anaelewa sababu ya chama kimoja ambacho hajakitaja, kimekataa kushiriki mchakato wa majadiliano ya kutafuata muafaka mazingira ya ufanyaji siasa na kuleta umoja wa kitaifa nchini. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Rais Samia ameyasema hayo jioni ya Jumamosi tarehe 23 Aprili, 2022 wakati akizungumza na Watanzania waishio Marekani (Diaspora), Washington DC na kueleza kuwa bado anaendelea na majadiliano nao ili wajiunge na wenzao.

“Tumeanza mazungumzo na vyama vya siasa kupitia baraza lao la siasa tumefamnya mkutano wa awali na kuunda kikosi kazi chao wenyewe watajadili mambo ambayo wenyewe wamepanga watatuletea.

“Kuna chama cha siasa kimoja bado hakijakubali, bado naendelea na mazungumzo nao na naelewa kwanini hawajakubali moja kwa moja kujiunga bado naendelea na mazungumzo nao tunakwenda vizuri na namatumaini watajiunga na wenzao,” amesema Rais Samia.

Rais Samia ambaye alipokewa na mabango na baadhi ya Watanzania waliokuwa wakipeleka ujumbe wa kutaka mchakato wa Katiba mpya amesema, “hali ya kiisasa tupo viruri mambo yote wanazungumza kikosi kazi watatuletea.”

Chama Cha Demokrasia na Maendeleo Chadema ndicho amabcho hakikushiriki mikutano na makongamano yote yalioandaliwa na Kituo cha Demokrasia Tanzania n ahata yale ya Baraza la Vyama Vya Siasa.

Chadema wamekuwa na msimamo huo kwa kile wanachodai kuwa mchakato huo hauna nia ya dhati ya kupatikana kwa Katiba Mpya kabla ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025.

Chama hicho kikuu cha upinzani mara baada ya uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020 kilitoa tamko la kutoshiriki uchaguzi wowote nchini hadi pale Katiba Mpya itakapopatikana.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!