Friday , 17 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa UN yazigeukia nchi za Afrika msimamo vita Ukrenia
Kimataifa

UN yazigeukia nchi za Afrika msimamo vita Ukrenia

Spread the love

 

BALOZI wa Marekani katika Umoja wa Mataifa , amesema kuwa mataifa ya Afrika hayawezi kubaki kutounga mkono upande wowote katika vita ya Ukraine. Inaripoti BBC.

Taarifa hiyo imekuja baada ya Linda Thomas – Greenfield kuzungumza na BBC na kubaini kuwa katika kura ,iliyopigwa kwenye mkutano wa Baraza Kuu, wiki mbili zilizopita zilionesha kuchukiwa kwa uvamizi wa Urusi dhidi ya Ukraine katika ,nchi 17 za Afrika, ambazo ni nusu ya Dunia nzima , zilijizuia na nyingine nane hazikupiga kura kabisa.

Hata hivyo Balozi huyo alisema kwamba hakuweza kuwa na msingi kwenye kutoegemea upande wowote , kwakuwa mgogoro huo haukuwa wa mashindano ya Vita Baridi kati ya nchi za Magharibi na Urusi .

Aidha Thomas -Greenfield amesema, Marekani ilikuwa ikisaidia kutafuta vyanzo mbadala vya bidhaa ambazo nchi huagiza kutoka Urusi.

Mwanadiplomasia huyo amesema kwamba Marekani itaunga mkono pendekezo la Afrika Kusini la Kupatanisha Urusi na Ukraine.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Bunge kumuweka katibu mkuu wa EAC kikaangoni

Spread the loveAliyekuwa Katibu mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Dk. Peter...

Kimataifa

Palestina mwanachama wa 194 wa UN

Spread the loveBaraza Kuu la Umoja wa Mataifa jana Ijumaa limepitisha kwa...

Habari za SiasaKimataifa

Israel yatia shubiri Gaza wakisherehekea Hamas kusitisha mapigano

Spread the loveWAKATI kundi la Hamas huko Gaza likitangaza kuridhia pendekezo lao...

KimataifaMakala & Uchambuzi

Mbivu, mbichi urais wa Ramaphosa mwezi huu

Spread the loveMWISHONI mwa mwezi huu, raia wa Afrika Kusini watapiga kura...

error: Content is protected !!