Thursday , 25 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Aliyewahi kuwa mkimbizi kutoka Burundi awachangia mahindi wakimbizi Ukraine
Kimataifa

Aliyewahi kuwa mkimbizi kutoka Burundi awachangia mahindi wakimbizi Ukraine

Spread the love

 

NCHINI Burundi Mkulima mdogo wa zao la Mahindi ametoa mchango wa kilo 100 za mahindi kwa wale waliokimbia ghasia nchi Ukraine.

Kijana huyo ambaye zamani alikuwa mkimbizi anayefahamika kwa jina la Adrien Nimpagaritse alikuwa yatima akiwa na umri wa miaka minne alipokimbilia nchini Tanzania, wakati wa wimbi la ghasia za kikabila mwaka 1996.

Alisema alilelewa katika kambi ya wakimbizi ya Mutenderi , ambako alisoma shule na kurejea nyumbani Burundi baada ya miaka 11 mwaka 2007 , akiwa na umri wa miaka 15 .

‘’Niliona jinsi wakimbizi wanavyokuwa wakiishi hatukuweza kupata chakula ‘’ alisema.

‘’Iwapo mtu , Jirani angekupa jani la muhogo tu au maji ungeshukuru sana ‘’

Hata hivyo Nimpagaritse sasa anaishi katika jimbo la Ruyingi mashariki mwa Burundi , ambako ameoa na kufanikiwa kupata Watoto watatu.

Kijana huyo mwenye umri wa miaka 30 alimtaka mtu kutoka shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi , kuja kuchukua mchango wake wa mahindi kwa ajili ya Ukraine .

Pia amesema yeye ana sauti ya kuchangia katika kuleta suluhu la mzozo huo, lakini anaweza kuchangia baadhi ya kile alichokilima kama ishara ya upendo.

Aidha amehimiza kama kuna mtu yeyote, aliye na moyo kama huo wa kusaidia tunaweza , kuwasaidia karibu familia 20.

‘’Binafsi ninaweza kumudu kutoa kilo 100 za mahidi , haitoshi ,kwa hivyo ikiwa kuna mtu mwingine ataongezea zaidi itasaidia’’

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!