Saturday , 18 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia atoa tahadhari mfumuko wa bei
Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia atoa tahadhari mfumuko wa bei

Spread the love

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan ametahadharisha uwepo wa mfumuko mkubwa wa bei nchini unaosababishwa na kupanda kwa bei ya mafuta duniani kutokana na vita inayoendelea kati ya Ukraine na Urusi. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Rais Samia ametoa tahadhari hiyo leo tarehe 8 Machi 2022, katika maadhimisho ya siku ya wanawake duniani yaliyofanyika katika viwanja vya Maisara Visiwani Zanzibar.

Mkuu huyo wa nchi amesema jinsi mafuta yanavyopanda bei, Tanzania haitanusurika kwani bidhaa zote zitapanda bei.

“Bidhaa zitapanda bei, nauli zitapanda bei, kila kitu kitapanda, thamani ya kila kitu itapanda kwasababu mafuta yanapanda bei,” amesema Rais Samia.

Aidha amesema kuna minong’ono imenza kusikika kuwa maisha yamekuwa magumu huku lawama zikipelekwa kwa viongozi kuwa hawana baraka.

“Si baraka ya kiongozi, ni hali ya ulimwengu inavyokwenda mafuta yanapanda bei duniani na bidhaa zote zitapanda bei,” amesisitiza.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

RC Chongolo atangaza ‘vita’ kwa wanaovusha wageni kinyemela

Spread the loveKATIKA kulinda usalama wa nchi kupitia mpaka wa Songwe, Mkuu...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

RUWASA yachongewa, yateketeza mamilioni kwa maji yenye magadi

Spread the loveSAKATA la ukosefu wa maji wilayani Momba mkoani Songwe limezidi...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Lissu akabidhiwa gari lake, aomba msaada wa matengenezo

Spread the loveMakamu Mwenyekiti wa Chadema Bara, Tundu Lissu leo Ijumaa amekabidhiwa...

Habari za SiasaTangulizi

Haya hapa majina walioteuliwa kugombea nafasi mbalimbali CHADEMA

Spread the loveCHAGUZI wa kanda za Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA)...

error: Content is protected !!