Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia atengua Ma-DED wanne
Habari za Siasa

Rais Samia atengua Ma-DED wanne

Rais Samia Suluhu Hassan
Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan ametangaza kutengua uteuzi wa wakurugenzi wanne wa halmashauri (DED) ya Buchosha (Mwanza), Iringa, Mbeya na Singida Mjini baada ya kubainika kutumia vibaya fedha za UVIKO-19. Anaripoti Mwandishi Wetu, Mwanza … (endelea).

Ametangaza uamuzi huo leo Ijumaa, tarehe 4 Februari 2022 akizungumza na wananchi wa Magu mkoani Mwanza akiwa njiani kwenda mkoani Mara katika ziara ya siku nne.

Rais Samia amesema, wakati anatangaza mgawanyo wa Sh.1.3 trilioni mkopo kutoka Shirika la Fedha Duniani (IMF) kugharamikia miradi mbalimbali ya maenfeleo, “nilisema kama mkurugenzi anataka kuona rangi yangu halisi achezee hizo fedha.”

Amesema wakurugenzi hao alitengua uteuzi wake anasubiri ripoti nyingine ya mkurugenzi wa Geita kutoka kwa timu yake pamoja na ile ya Waziri wa Tamisemi, Innocent Bashungwa.

“Wakurugenzi wa Buchosa, Iringa, Mbeya na Singida Mjini, nimewatengua sasa hivi na nasubiri ripoti yenu ila nimewatengua kabla ya ripoti yenu kwani mmekuwa na tabia ya kuwafichia fichia na yule wa Geita endeleeni na uchunguzi na mimi timu yangu inaendelea ikiniletea taarifa naye nitamtengua,” amesema Rais Samia

Mkuu huyo wa nchi amewaeleza wananchi kwamba, Serikali anayoingoza “imeapa kuleta maendeleo kwa wananchi hivyo wawaombee ili waweze kutekeleza hilo kwa ufanisi ili Tanzania iweze kustawi na kunawili.”

“Ndugu zangu kuna maneno yalizunguka zunguka kwamba hakuna elimu bure ni waongo, tumejenga vituo vya afya, walisema miradi mikubwa itasimama haijengwi imesimama, reli yetu ya SGR inajengwa na kufika 2025 roti tano zote zitakuwa zimejengwa,” amesema

Kuhusu Bwawa la Umeme la Mwalimu Nyerere, “bado linaendelea na ujenzi unafikia asilimia sitini na na ujenzi unaendelea na hatudaiwi. Tunawaomba wananchi wa Magu msidanganywe na sisi tutafanya kama walivyofanya watangulizi wetu.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za SiasaTangulizi

Samia awataka watanzania kudumisha muungano

Spread the loveRais wa Tanzania,Samia Suluhu Hassan amewataka Watanzania kuendeleza Muungano kwa...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

error: Content is protected !!