Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia atengua Ma-DED wanne
Habari za Siasa

Rais Samia atengua Ma-DED wanne

Rais Samia Suluhu Hassan
Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan ametangaza kutengua uteuzi wa wakurugenzi wanne wa halmashauri (DED) ya Buchosha (Mwanza), Iringa, Mbeya na Singida Mjini baada ya kubainika kutumia vibaya fedha za UVIKO-19. Anaripoti Mwandishi Wetu, Mwanza … (endelea).

Ametangaza uamuzi huo leo Ijumaa, tarehe 4 Februari 2022 akizungumza na wananchi wa Magu mkoani Mwanza akiwa njiani kwenda mkoani Mara katika ziara ya siku nne.

Rais Samia amesema, wakati anatangaza mgawanyo wa Sh.1.3 trilioni mkopo kutoka Shirika la Fedha Duniani (IMF) kugharamikia miradi mbalimbali ya maenfeleo, “nilisema kama mkurugenzi anataka kuona rangi yangu halisi achezee hizo fedha.”

Amesema wakurugenzi hao alitengua uteuzi wake anasubiri ripoti nyingine ya mkurugenzi wa Geita kutoka kwa timu yake pamoja na ile ya Waziri wa Tamisemi, Innocent Bashungwa.

“Wakurugenzi wa Buchosa, Iringa, Mbeya na Singida Mjini, nimewatengua sasa hivi na nasubiri ripoti yenu ila nimewatengua kabla ya ripoti yenu kwani mmekuwa na tabia ya kuwafichia fichia na yule wa Geita endeleeni na uchunguzi na mimi timu yangu inaendelea ikiniletea taarifa naye nitamtengua,” amesema Rais Samia

Mkuu huyo wa nchi amewaeleza wananchi kwamba, Serikali anayoingoza “imeapa kuleta maendeleo kwa wananchi hivyo wawaombee ili waweze kutekeleza hilo kwa ufanisi ili Tanzania iweze kustawi na kunawili.”

“Ndugu zangu kuna maneno yalizunguka zunguka kwamba hakuna elimu bure ni waongo, tumejenga vituo vya afya, walisema miradi mikubwa itasimama haijengwi imesimama, reli yetu ya SGR inajengwa na kufika 2025 roti tano zote zitakuwa zimejengwa,” amesema

Kuhusu Bwawa la Umeme la Mwalimu Nyerere, “bado linaendelea na ujenzi unafikia asilimia sitini na na ujenzi unaendelea na hatudaiwi. Tunawaomba wananchi wa Magu msidanganywe na sisi tutafanya kama walivyofanya watangulizi wetu.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

CAG aibua madudu halmashauri 10, TANESCO na MSD

Spread the loveRIPOTI ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali...

Habari za Siasa

Alichokisema Rais Samia baada ya kupokea ripoti ya CAG, TAKUKURU

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Serikali yake itafanyia kazi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

Habari za SiasaTangulizi

Deni la Serikali laongezeka kwa trilioni 11

Spread the loveDENI la Serikali imeongezeka kwa takribani Sh. 11 trilioni sawa...

error: Content is protected !!