Sunday , 19 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mrithi wa Maalim Seif atema cheche
Habari za SiasaTangulizi

Mrithi wa Maalim Seif atema cheche

Spread the love

 

MWENYEKITI mpya wa chama cha upinzani nchini Tanzania-ACT Wazalendo, Juma Duni Haji maarufu Babu Duni amewashukuru wote waliomchagua kushika wadhifa huo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Babu Duni amechaguliwa na wajumbe wa mkutano mkuu maalum wa ACT-Wazalendo uliofanyika jana Jumamosi, tarehe 29 Januari 2022, kwa kura 339 sawa na asilimia 73.06 ya kura zote 468.

Mshindani wake wa karibu alikuwa waziri wa zamani wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar akipata kura 125 sawa na asilimia 26.

Babu Duni amechukua nafasi iliyoachwa wazi na mkongwe mwenzake wa siasa hususan Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad ambaye alifariki dunia tarehe 17 Februari 2021, katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) alikokuwa akipatiwa matibabu.

Baada ya kutangazwa mshindi, Babu Dunia alizungumza na wajumbe wa mkutano huo na kuelezea anachokwenda kukifanya.

Fuatilia hotuba yake yote aliyoitoa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

CCM yamteua Pele kuwa mgombea ubunge Kwahani

Spread the loveKamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM)...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Ujenzi kituo cha kupoza umeme Chalinze wafikia asilimia 93.7

Spread the loveKamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imeeleza...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Wakili Mwabukusi anusurika kufungiwa, asema hatarudi nyuma

Spread the loveWAKILI Boniface Mwabukusi amesema kuwa hatorudi nyuma kuwatetea Watanzania na...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

RC Chongolo atangaza ‘vita’ kwa wanaovusha wageni kinyemela

Spread the loveKATIKA kulinda usalama wa nchi kupitia mpaka wa Songwe, Mkuu...

error: Content is protected !!