Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Tangulizi AG wa zamani aapishwa kuwa Balozi, Nchimbi…
Tangulizi

AG wa zamani aapishwa kuwa Balozi, Nchimbi…

Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amemwapisha Profesa Adelardus Kilangi kuwa Balozi wa Tanzania nchini Brazil. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Profesa Kilangi, ameapishwa leo Jumatatu, tarehe 6 Desemba 2021, Ikulu jijini Dar es Salaam.

Anakwenda kuchukua nafasi ya Emmanuel Nchimbi ambaye alihudumu nafasi hiyo kuanzia Februari 2017, baada ya kuteuliwa na aliyekuwa Rais wa wakati huo, Hayati John Pombe Magufuli.

Haijafahamika, kama Nchimbi ambaye amewahi pia kuwa waziri wa mambo ya ndani katika utawala wa awamu ya nne chini ya Rais Jakaya Kikwete, anarejea nchini au amepangiwa kituo kingine cha kazi.

Kabla ya kuteuliwa kwa Profesa Kilangi kuwa Balozi, tarehe 12 Septemba 2021, alikuwa mwanasheria mkuu wa serikali (AG).

Nafasi hiyo ya mwanasheria mkuu wa serikali, aliteuliwa Dk. Eliezer Feleshi, ambaye alikuwa Jaji Kiongozi wa Tanzania.

Profesa Kilangi, aliteuliwa kuwa mwanasheria mkuu wa serikali, tarehe 1 Februari 2018, akichukua nafasi ya George Masaju, aliyeteuliwa kuwa Jaji wa Mahakama Kuu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kwafukuta kisa chaguzi, Lissu aibua tuhuma nzito

Spread the loveCHAGUZI za kusaka viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo...

Habari MchanganyikoTangulizi

Kimbunga “HIDAYA” chaendelea kuimarika, wananchi wapewa tahadhari

Spread the loveMAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inaendelea kutoa taarifa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali yaanza msako wanaotoa mikopo kausha damu

Spread the loveSERIKALI imeanza kufuatilia watu, vikundi na taasisi zinazotoa kinyume cha...

error: Content is protected !!