Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Tangulizi AG wa zamani aapishwa kuwa Balozi, Nchimbi…
Tangulizi

AG wa zamani aapishwa kuwa Balozi, Nchimbi…

Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amemwapisha Profesa Adelardus Kilangi kuwa Balozi wa Tanzania nchini Brazil. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Profesa Kilangi, ameapishwa leo Jumatatu, tarehe 6 Desemba 2021, Ikulu jijini Dar es Salaam.

Anakwenda kuchukua nafasi ya Emmanuel Nchimbi ambaye alihudumu nafasi hiyo kuanzia Februari 2017, baada ya kuteuliwa na aliyekuwa Rais wa wakati huo, Hayati John Pombe Magufuli.

Haijafahamika, kama Nchimbi ambaye amewahi pia kuwa waziri wa mambo ya ndani katika utawala wa awamu ya nne chini ya Rais Jakaya Kikwete, anarejea nchini au amepangiwa kituo kingine cha kazi.

Kabla ya kuteuliwa kwa Profesa Kilangi kuwa Balozi, tarehe 12 Septemba 2021, alikuwa mwanasheria mkuu wa serikali (AG).

Nafasi hiyo ya mwanasheria mkuu wa serikali, aliteuliwa Dk. Eliezer Feleshi, ambaye alikuwa Jaji Kiongozi wa Tanzania.

Profesa Kilangi, aliteuliwa kuwa mwanasheria mkuu wa serikali, tarehe 1 Februari 2018, akichukua nafasi ya George Masaju, aliyeteuliwa kuwa Jaji wa Mahakama Kuu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia ataja mikakati ya kufikia trilioni 2 biashara Uturuki, Tz

Spread the loveWakati Tanzania na Uturuki zikidhamiria kuongeza kiwango cha biashara hadi...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Habari za SiasaTangulizi

Tanzania, Uturuki zanuia kukuza biashara, uwekezaji

Spread the loveSERIKALI za Tanzania na Uturuki zimekubaliana kuendeleza dhamira ya kuimarisha...

error: Content is protected !!