Saturday , 18 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia amwapisha Silima kuwa Balozi wa Comoro
Habari za Siasa

Rais Samia amwapisha Silima kuwa Balozi wa Comoro

Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amemuapisha Pereira Ame Silima (62) kuwa Balozi wa Tanzania nchini Comoro. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Silima ameapishwa leo Jumapili, tarehe 7 Novemba 2021, Ikulu ya Chamwino jijini Dodoma kuchukua nafasi ya Sylvester Mabumba ambaye haijaelezwa amestaafu au atapangiwa majukumu mengine.

Amewahi kuwa Mbunge wa Chumbani visiwani Zanzibar. Aidha, akiwa mbunge alipata fursa kuhudumu nafasi ya naibu waziri wa mambo ya ndani na naibu waziri wa wizara ya fedha.

Katika uchaguzi mkuu uliopita wa Oktoba 2020, Silima alijitosa kwenye mbio za urais ndani ya chama tawala- Chama Cha Mapinduzi (CCM), Zanzibar kutaka kuchukua nafasi iliyokuwa inaachwa wazi na Dk. Ali Mohamed Shein.

Hata hivyo, mwisho wa kinyyng’anyiro hicho, Dk. Hussein Ali Mwinyi alipitishwa na Halmashauri Kuu ya CCM kupeperusha bendera ya chama hicho na baadaye kwenye uchaguzi mkuu uliofanyika 27 na 28 Oktoba 2021, akashinda uchaguzi mkuu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Wakili Mwabukusi anusurika kufungiwa, asema hatarudi nyuma

Spread the loveWAKILI Boniface Mwabukusi amesema kuwa hatorudi nyuma kuwatetea Watanzania na...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

RC Chongolo atangaza ‘vita’ kwa wanaovusha wageni kinyemela

Spread the loveKATIKA kulinda usalama wa nchi kupitia mpaka wa Songwe, Mkuu...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

RUWASA yachongewa, yateketeza mamilioni kwa maji yenye magadi

Spread the loveSAKATA la ukosefu wa maji wilayani Momba mkoani Songwe limezidi...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Lissu akabidhiwa gari lake, aomba msaada wa matengenezo

Spread the loveMakamu Mwenyekiti wa Chadema Bara, Tundu Lissu leo Ijumaa amekabidhiwa...

error: Content is protected !!