Saturday , 27 April 2024
Home Kitengo Michezo Alikiba: Mfalme ni mmoja tu, albam wiki ijayo
Michezo

Alikiba: Mfalme ni mmoja tu, albam wiki ijayo

Ali Kiba
Spread the love

 

HATIMAYE Staa wa Bongofleva nchini, Ali Salehe Kiba maarufu kama Alikiba ametangaza kuachia albam yake ya tatu inayokwenda kwa jina la ‘The Only King. Anaripoti Matilda Buguye na Patricia Kighono, TUDARCo … (endelea).

Akizungumza na waandishi wa habari leo tarehe 29 Septemba 2021 jijini Dar es Salaam, Alikiba amesema albam hiyo ataiachia tarehe 7 Oktoba mwaka huu.

Amesema albam hiyo yenye nyimbo 16, amechagua kuipa jina hilo la The Only King kwani ndilo jina linaloendana na hisia za mashabiki wake na nafasi yake kwenye Bongofleva.

Pia ameongeza kuwa amechagua jina hilo kwa sababu mfalme ni moja tu na hakuna wafalme wawili kwa maana hiyo yeye atabaki kuwa mfalme kwenye Bongo fleva ambayo amedumu kwa muda wa miaka 19 mfululizo.

Aidha, Kiba amesema ndani ya albam hiyo ameshirikisha wasanii mbalimbali kutoka Barani Afrika.

“Albam hii ilihitaji maandalizi makubwa ndio maana nilichelewa kuitoa licha ya kuitambulisha kwa muda mrefu.

“Lebo yetu ya Kings music imeshirikiana na Ziik ambayo ni kampuni ya kuuza muziki katika kuandaa albam hiii hivyo mashabiki wangu watarajie mambo makubwa,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!