Sunday , 28 April 2024
Home Kitengo Michezo Mwili wa Hans Pope kuagwa Dar, kuzikwa Iringa J’tano
Michezo

Mwili wa Hans Pope kuagwa Dar, kuzikwa Iringa J’tano

Marehemu Zacharia HansPope
Spread the love

 

MWILI wa Zacharia Hans Pope, mjumbe wa bodi ya wakurugenzi wa timu ya Simba nchini Tanzania utaagwa kesho Jumatatu, tarehe 13 Septemba 2021, ukumbi wa Karimjee, jijini Dar es Salaam. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Hans Pope, ambaye pia alikuwa mjumbe wa kamati ya sharia, hadhi na madaraka ya wachezaji alifariki dunia usiku wa Ijumaa tarehe 10 Septemba 2021, katika Hospitali ya Agha Khan jijini Dar es Salaam jijini humo alipokuwa akipatiwa matibabu.

Ratiba iliyotolewa na mabingwa wa ligi kuu Tanzania bara 2020/21, Simba inaonesha mwili wa Hans Pope utazikwa kijijini kwao, Kihesa Mkimbizi mkoani Iringa.

Mbali na kujihusisha na masuala ya michezo, Hans Pope aliyekuwa mwenyekiti wa kamati ya usajili wa Simba aliwahi kuwa Luteni wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), akiwa miongoni mwa waliotaka kufanya jarabio la kumpindua Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, lakini wakashindwa.

Hatua hiyo, ilimfanya Hans Pope na wenzake kutupwa gerezani hadi mwaka 1995 walipokuja kuachiwa na Rais wa wakati huo, Ali Hassan Mwinyi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Beti na Meridianbet mechi za leo

Spread the love IKIWA leo hii ni Jumapili tulivu kabisa, Meridianbet wanamkwambia...

Michezo

Jumamosi ya leo ni ya pesa tu kutoka Meridianbet

Spread the love  IKIWA leo hii ni Jumamosi nyingine na tulivu kabisa,...

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

error: Content is protected !!