Thursday , 9 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Tukio la risasi Dar; IGP Sirro asema askari wawili wafariki dunia
Habari Mchanganyiko

Tukio la risasi Dar; IGP Sirro asema askari wawili wafariki dunia

IGP Simon Sirro
Spread the love

 

INSPEKTA Jenerali wa Polisi (IGP), Simon Sirro amesema, askari wawili wamefariki dunia wakati wakimdhibiti mtu mmoja aliyekuwa alifyatua risasi hovyo karibu na Ubalozi wa Ufarasa, Dar es Salaam leo mchana. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

IGP Sirro amesema, mtu huyo naye amefariki dunia kwenye majibizano ya risasi kati yake na askari.

Tukio hilo limetokea mchana wa leo Jumatano, tarehe 25 Agosti 2021, karibu na Ubalozi wa Ufaransa jijini Dar es Salaam na kusababisha taharuki kwa wananchi.

Picha na vipande mbalimbali vya video, vimesambaa mitandaoni vikionyesha mtu huyo akiwa na silaha mbili, moja ikining’inia shingoni na nyingine ameishika mkononi.

James Kolnel, kondakta wa daladala kutoka Makumbusho kwenda Posta, aliyekuwa eneo la tukio amesema “baada ya kuona risasi zinazidi nikaamua kufungua mlango nikawaambia abiria tokeni nje mjitetee wenyewe maana hali halisi mnaiyona.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoMichezo

Kengold wakabidhiwa kombe NBC Championship

Spread the loveMdhamini mkuu wa Ligi Daraja la Kwanza (NBC Championship) Benki...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Rais Samia: Matumizi ya nishati safi sio anasa, ladha ipo

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amesema matumizi ya nishati safi kwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC, SILABU waungana kufikisha elimu ya fedha majumbani

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imeingia makubaliano ya ushirikiano...

AfyaHabari MchanganyikoMakala & Uchambuzi

Kisukari cha mimba ni nini?

Spread the loveKisukari cha mimba ni aina ya kisukari kinachotokea kwa baadhi...

error: Content is protected !!