Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Tukio la risasi Dar; IGP Sirro asema askari wawili wafariki dunia
Habari Mchanganyiko

Tukio la risasi Dar; IGP Sirro asema askari wawili wafariki dunia

IGP Simon Sirro
Spread the love

 

INSPEKTA Jenerali wa Polisi (IGP), Simon Sirro amesema, askari wawili wamefariki dunia wakati wakimdhibiti mtu mmoja aliyekuwa alifyatua risasi hovyo karibu na Ubalozi wa Ufarasa, Dar es Salaam leo mchana. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

IGP Sirro amesema, mtu huyo naye amefariki dunia kwenye majibizano ya risasi kati yake na askari.

Tukio hilo limetokea mchana wa leo Jumatano, tarehe 25 Agosti 2021, karibu na Ubalozi wa Ufaransa jijini Dar es Salaam na kusababisha taharuki kwa wananchi.

Picha na vipande mbalimbali vya video, vimesambaa mitandaoni vikionyesha mtu huyo akiwa na silaha mbili, moja ikining’inia shingoni na nyingine ameishika mkononi.

James Kolnel, kondakta wa daladala kutoka Makumbusho kwenda Posta, aliyekuwa eneo la tukio amesema “baada ya kuona risasi zinazidi nikaamua kufungua mlango nikawaambia abiria tokeni nje mjitetee wenyewe maana hali halisi mnaiyona.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!