Tuesday , 21 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa NEC : Jimbo la Konde liko wazi
Habari za Siasa

NEC : Jimbo la Konde liko wazi

Mkurugenzi wa Uchaguzi wa NEC, Dk. Wilson Mahera
Spread the love

 

TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), imetangaza Jimbo la Konde visiwani Zanzibar, liko wazi baada ya mbunge wake mteule kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Sheha Mpemba Faki, kujiuzulu kwa sababu za kifamilia. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Taarifa hiyo imetolewa jana tarehe 2 Julai 2021 na Mkurugenzi wa Uchaguzi NEC, Dk. Wilson Mahera, baada ya Faki kujuzulu nafasi hiyo.

Taarifa ya Mahera imesema kuwa, NEC imeamua kutangaza jimbo hilo kuwa wazi, baada ya kupokea taarifa kutoka kwa Katibu Mkuu wa CCM, Daniel Chongolo, juu ya uamuzi wa mwanachama wake kujiuzulu ubunge.

“NEC imepokea barua kutoka kwa Katibu Mkuu wa CCM yenye Kumb. Na. CCM/T.40/8vol.1/72, ya tarehe 2 Agosti 2021, ikitoa taarifa kuwa Mbunge mteule wa Konde, Faki aliandika barua kwa chama hicho kukitaarifu kuwa hayupo tayari kuwawakilisha wananchi wa Konde katika Bunge , kutokana na changamoto za kifamilia,” imesema taarifa ya Dk. Mahera.

 

Sheha Mpemba Faki

Taarifa hiyo imesema, taratibu za kujaza nafasi hiyo zitatangazwa baadae.

“Kutokana na hatua hiyo, tume inatoa taarifa kwa umma kuwa Jimbo la Konde lipo wazi na taratibu za kujaza nafasi hiyo zitatangazwa hivi karibuni. Tume imefanya hivyo kwa kuwa ilikuwa bado haijamjulisha Spika wa Bunge, kuhusu kukamilika kwa uchaguzi huo na kuchaguliwa kwa Faki,” imesema taarifa ya Dk. Mahera.

Faki alijiuzulu nafasi hiyo siku 15 baada ya kutangazwa mshindi wa uchaguzi mdogo wa Jimbo la Konde, uliofanyika tarehe 18 Julai 2021, baada ya aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo, Khatib Said Haji kupitia ACT-Wazalendo, kufariki dunia.

Katika uchaguzi huo, Faki alimbwaga aliyekuwa mgombea wa ACT-Wazalendo, Mohammed Said Issa.
Haji aliyeliongoza jimbo hilo kwa zaidi ya miaka 10 akiwa Chama cha Wananchi (CUF) na ACT-Wazalendo, alifariki dunia tarehe 20 Mei 2021, katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, alikokuwa anapatiwa matibabu.

1 Comment

  • ccm kwa kushirikiana na tume ya uchafuzi na ccmjeshpolisi walishirikiana kupora ushindi wa mgombea wa ACT Wazalendo. Acheni kutafuna maneno semeni ukweli wa mambo kwamba faki mpemba hakushinda uchaguzi ila tume pamoja na jeshi la polisi walipora ushindi wa mgombea wa ACT WANZALENDO, Tunataka walioshiriki kuharibu uchaguzi wawajibishwe ili raia warudishe imani kwa tume ya uchaguzi visiwani. Haitoshi kuwa wazi jimbo la konde pesa zilizotumika sio nyele za wilson mahera ni kodi ya wananchi lazima waliohusika wawajibishwe ili iwe fundisho.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Balozi Nchimbi aonya maofisa utumishi kuacha uonevu

Spread the loveKatibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dk. Emmanuel...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Balozi Kasike ateta na mjumbe wa FRELIMO

Spread the loveBalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Msumbiji, Phaustine...

Habari za SiasaKimataifa

Kiongozi Mkuu Iran amteua mrithi wa Rais Ebrahim

Spread the loveKiongozi wa ngazi ya juu nchini Iran, Ayatollah Ali Khamenei,...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Watumishi 85,471 walioenguliwa kipindi cha JPM wapandishwa vyeo

Spread the loveSERIKALI imesema kuanzia mwaka wa fedha 2021/2022 hadi sasa jumla...

error: Content is protected !!