Sunday , 19 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Bunge: Wabunge Tanzania wanalipa kodi
Habari za Siasa

Bunge: Wabunge Tanzania wanalipa kodi

Bunge la Tanzania
Spread the love

 

OFISI ya Bunge la Tanzania imesema, wabunge kama ilivyo kwa watumishi wengine wa umma na viongozi wa kisiasa nchini humo, wanakatwa kodi zote stahiki kwa mujibu wa sheria. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Miongoni mwa kodi hizo ni kodi ya mapato (PAYE), inayokatwa kwenye mishahara ya wabunge ya kila mwezi.

Taarifa ya Kitengo cha Mawasiliano na Uhisiano wa Kimataifa ya Bunge la Tanzania, iliyotolewa leo Jumanne, tarehe 3 Agosti 2021, imesema kinachoendelea kitandaoni kwamba wabunge hawalipi kodi kwenye mishahara hao hakina ukweli.

Ofisi hiyo ya Bunge, imetoa ufafanuzi huo baada ya siku za hivi karibuni, kuibuka taarifa mitandaoni kwamba, wabunge hawalipi kodi hivyo maumivu wanayoyapata kupitia tozo za miamala ya simu hawahusiki nayo.

Tozo hizo, zilianza kutumika tarehe 15 Julai 2021, baada ya kupitishwa na Bunge. Tozo hizo zimekuwa zikilalamikiwa na wananchi kwamba zinawaumiza na tayari Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, ameagiza zipitiwe upya kuangalia kama zinaweza kupunguzwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Wakili Mwabukusi anusurika kufungiwa, asema hatarudi nyuma

Spread the loveWAKILI Boniface Mwabukusi amesema kuwa hatorudi nyuma kuwatetea Watanzania na...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

RC Chongolo atangaza ‘vita’ kwa wanaovusha wageni kinyemela

Spread the loveKATIKA kulinda usalama wa nchi kupitia mpaka wa Songwe, Mkuu...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

RUWASA yachongewa, yateketeza mamilioni kwa maji yenye magadi

Spread the loveSAKATA la ukosefu wa maji wilayani Momba mkoani Songwe limezidi...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Lissu akabidhiwa gari lake, aomba msaada wa matengenezo

Spread the loveMakamu Mwenyekiti wa Chadema Bara, Tundu Lissu leo Ijumaa amekabidhiwa...

error: Content is protected !!