Saturday , 4 May 2024
Home Kitengo Michezo Yanga yamlilia Kenneth Kaunda
Michezo

Yanga yamlilia Kenneth Kaunda

Hayati Keneth Kaunda
Spread the love

 

MABINGWA wa Kihistoria nchini Tanzania, Yanga ya Dar es Salaam, imetoa salamu za rambirambi, kufuatia kifo cha Kenneth Kaunda, Rais wa kwanza wa Zambia. Anaripoti Kelvein Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Kaunda (97), alifikwa na mauti jana Alhamisi, tarehe 17 Juni 2021, katika moja ya hospitali mjini Lusaka, Zambia alipokuwa akipatiwa matibabu.

Tangu kutokea kwa kifo hicho, salamu mbalimbali zimeendelea kutolewa ikiwemo Klabu ya Yanga ambayo uwanja wake wa mazoezi ulipo makao makuu, unatitwa Kaunda, rais huyo aliyoongoza Zambia kwa miaka 27 kuanzia 1964 hadi 1991.

“Salama za Rambirambi. Pumzika kwa amani Rais wa kwanza na Muasisi wa Taifa la Zambia Hayati Kenneth Kaunda.”

“Klabu ya Yanga SC itaendelea kumkumbuka na kumuenzi Hayati Keneth Kaunda kwa kuhakikisha Uwanja wa Kaunda uliopo Makao Makuu ya Klabu, Jangwani unaendelezwa ikiwa ni sehemu muhimu ya kumbukumbu yake katika Historia ya Klabu yetu,” imeandika Yanga katika akaunti zake za kijamii

Hata hivyo, kwa sasa Uwanja huo wa Kaunda, haufanyi kazi, kwani kuna vifusi vimewekwa kwa kipindi kirefu kwa kile kinachosubiriwa kufanyiwa ukarabati mkubwa ili kuuwezesha kutumika.

Mara kadhaa, uwanja huo, umekuwa ukijaa maji pindi mvua inaponyesha kutokana na kuwa bondeni.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Ligi mbalimbali za pesa kuendelea leo

Spread the love Ijumaa ya leo ambapo mechi mbalimbali zinaendelea Duniani Meridianbet...

Michezo

Europa na Conference kukupatia pesa ndefu leo

Spread the love  ALHAMISI ya leo tutaenda kushuhudia mitanange ya kukata na...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

Michezo

Usiku wa Ulaya umerejea kibabe kabisa

Spread the love  LIGI ya Mabingwa barani Ulaya imerejea tena na awamu...

error: Content is protected !!