Saturday , 4 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Serikali yaanza kukamilisha mfumo wa gesi asilia
Habari Mchanganyiko

Serikali yaanza kukamilisha mfumo wa gesi asilia

Moja ya kituo cha gesi asilia
Spread the love

 

SERIKALI ya Tanzania, kupitia Shirika la Petroli Tanzania (TPDC) linaendelea na kazi ya ujenzi wa miundombinu ya kusambaza gesi asilia katika mikoa mbalimbali. Anaripoti Nasra Bakari, DMC … (endelea).

Hayo yamesemwa leo Jumanne, tarehe 11 Mei, 2021, bungeni jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Nishati, Steven Byabato, alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum, Tunza Malapo.

“Je, ni lini serikali itaunganisha mfumo wa gesi asilia, kwa ajili ya kupata nishati ya kukaangia samaki katika soko la feri katika Manispaa ya Mtwara Mikindani?” ameuliza Malapo.

Byabato amejibu, Serikali inaendelea na kazi ya ujenzi wa miundombinu ya kusambaza gesi asilia katika mkoa wa Mtwara kwa ajili ya matumizi ya viwandani, majumbani na taasisi za umma na binafsi.

Amesema, katika mkoa wa Mtwara, mradi huu unahusisha ujenzi wa miundombinu ya kusambaza gesi asilia, kwa njia ya mabomba na vituo vya kuongeza mgandamizo wa gesi (Compressed Natural Gas (CNG) Station).

“Ujenzi wa miundombinu ya usambazaji wa gesi asilia katika soko la feri, Manispaa ya Mtwara Mikindani, upo katika hatua ya kukamilisha usanifu wa kina wa kihandisi, utakaofuatiwa na hatua ya kumpata mkandarasi wa ujenzi wa mradi huo.

“Kazi ya usanifu inatarajiwa kukamilika mwezi Agosti 2021, na ujenzi kuanza Desemba 2021, na kukamilika Juni 2022, gharama za mradi huu ni takribani Sh. 10.11 bilioni,” amesema Byabato.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

RPC Dodoma akabidhiwa bunduki mbili za wahalifu

Spread the love  Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa ya Kulevya...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yazindua huduma maalum kwa wastaafu

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imezindua huduma maalum kwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yazindua akaunti ya Kikundi

Spread the loveBenki ya NMB imezindua akaunti ya kikundi yenye  maboresho makubwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyakazi waidai STAMICO mishahara ya bilioni 1

Spread the loveWALIOKUWA wafanyakazi wa mgodi wa Shirika la Madini la Taifa...

error: Content is protected !!