Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Ndugai ashauri HESLB itoe mikopo vyuo vya kati, ufundi
Habari za Siasa

Ndugai ashauri HESLB itoe mikopo vyuo vya kati, ufundi

Bodi ya Mikopo Elimu ya Juu
Spread the love

 

SPIKA wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai, ameishauri Serikali ifanye marekebisho ya Sheria ya Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu (HESLB), ili itoe huduma kwa wanafunzi wa vyuo vya kati na ufundi stadi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Spika Ndugai ametoa wito huo leo Jumanne, tarehe 11 Mei 2021, jijini Dosoma, katika kilele cha mashindano ya kitaifa ya sayansi, teknolojia na ubunifu, yaliyohusisha wanafunzi wa vyuo vikuu na vya kati pamoja na shule za msingi na sekondari.

“Serikali iangalie ule mfuko unaosaidi wanafunzi wa elimu ya juu, sheria yake tuiangalie upya Serikali na Bunge ili badala kuangalia elimu ya juu pekee yake tuangalie wananfunzi wa vyuo vya kati vinavyotawaliwa na NACTE na VETA ili wanaofanya sayansi na teknolojia katika maeneo hayo waweze nufaika na mikopo badala ya wanafunzi wa vyuo pekee yake,” amesema Spika Ndugai.

Pia, Spika Ndugai amesema, mabadiliko hayo yawezeshe uwiano wa utoaji mikopo kwa wanafunzi wanaosoma masomo ya sayansi na sanaa.

Job Ndugai Spika wa Bunge la jamhuri ya muungano wa Tanzania

“Tuweke uwiano wa wanafunzi, tuiwekee msisitizo bodi yetu ya mikopo ya elimu juu ili asilimia 60 hadi 70 iende kwa wanafunzi wa sayansi na asilimis 40 iende kwa wengine. Ni wakati wa kubadili ratio (uwiano) ya mikopo inavyoenda,” amesema Spika Ndugai.

Wakati huo huo, Spika Ndugai ameshauri taasisi zinazofanya utafiti, ziongeze nguvu katika tafiti zinazohusiana na ukuaji wa uchumi wa wananchi.

“Watafiti nchini ikiwemo wa mazao ya kilimo wajitahidi kufanya tafiti zinazohusiana na ukuaji uchumi wa nchi yetu, uwafikie walengwa. Kwa kupitia tafiti hizo itasaida kusonga mbele, tuwe na tafiti nyingi zinazohusiana na maendeleo ya wananchi,” amesema Spika Ndugai.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!