Tuesday , 21 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mzee Mwinyi atimiza miaka 96, kuzindua kitabu chake leo
Habari za SiasaTangulizi

Mzee Mwinyi atimiza miaka 96, kuzindua kitabu chake leo

Spread the love

 

MZEE Ali Hassan Mwinyi, Rais mstaafu wa awamu ya pili wa Tanzania, leo Jumamosi, tarehe 8 Mei 2021, ametimiza miaka 96. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Mwinyi aliyeongoza kwa miaka kumi 1985-1995, alizaliwa tarehe 8 Mei 1925, Kivure, mkoani Pwani.

Anaitumia siku hii ya kuzaliwa kwake, kuzindua kitabu kinachoitwa “Mzee Rukhsa: Safari ya Maisha Yangu” ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam.”

Uzinduzi huo, utakaofanyika ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam, unatarajiwa kuhudhuliwa na viongozi mbalimbali, akiwemo Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan.

Wengine watakaohudhulia ni; Rais wa Zanzibar, Hussein Ali Mwinyi, Rais mstaafu wa Tanzania, Jakaya Kikwete.

Wengine ni marais wastaafu wa Zanzibar, Aman Abeid Karume, Dk. Ali Mohamed Shein pamoja na viongozi waandamizi wa sekta mbalimbali ikiwemo wale wa dini, siasa na asaso za kiraia.

Itakuwa ni kitabu cha pili kuzinduliwa, kikitanguliwa na cha Hayati Benjamin Wilium Mkapa, aliyekuwa Rais wa Tanzania kati ya mwaka 1995-2005 , kinachoitwa My Life, My Purpose “Maisha Yangu, Kusudio Langu” kilichozinduliwa tarehe 12 Novemba 2019.

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaKimataifaTangulizi

Waliowekewa damu yenye VVU, homa ya ini kulipwa fidia trilioni 32.9

Spread the loveWaziri mkuu wa Uingereza, Rishi Sunak ameahidi kulipa fidia ya...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali yanawa mikono fidia Kimara-Kibamba

Spread the loveSERIKALI imewataka waathiriwa wa bomoabomoa ya upanuzi wa barabara ya...

Habari za Siasa

Watumishi 25,039, taasisi 65 wahamia Dodoma

Spread the loveSerikali imesema hadi sasa, jumla ya watumishi 25,039 kutoka Serikali...

Habari za SiasaKimataifa

Balozi Kasike ateta na mjumbe wa FRELIMO

Spread the loveBalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Msumbiji, Phaustine...

error: Content is protected !!