Saturday , 4 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mnyika: Rais Samia amejibu barua ya Mbowe
Habari za SiasaTangulizi

Mnyika: Rais Samia amejibu barua ya Mbowe

Rais Samia Suluhu Hassan
Spread the love

 

JOHN Mnyika, Katibu Mkuu wa Chama Kikuu cha Upinzani Tanzania- Chadema amesema, Rais wa nchi hiyo, Samia Suluhu Hassan, amekubali wito wa chama hicho, kukutana na kushauri mambo mbalimbali. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Ni baada ya Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, kuueleza ulimwengu kuwa, wamemwandikia barua Rais Samia ya kuomba kuonana naye.

Mbowe aliyasema hayo tarehe 11 Aprili 2021, alipozungumza na Watanzania kupitia vyombo vya habari, kuhusu mambo kadhaa ikiwemo kifo cha aliyekuwa Rais wa Tanzania, John Pombe Magufuli.

Hayati Magufuli, alifariki dunia tarehe 17 Machi 2021, katika Hospitali ya Mzena, Dar es Salaam na mwili wake, kuzikwa nyumbani kwao Chato mkoani Geita 26 Machi 2021.

Mara baada ya kifo hicho, Samia aliyekuwa makamu wa Rais, aliapishwa kuwa Rais kwa mujibu wa Katiba ya Tanzania.

Katika maelezo yake Mbowe aliyoyatoa, alisema, Chadema imemwandikia barua Rais Samia ya kuomba kuona naye ili wazungumze masuala mbalimbali yenye manufaa kwa Taifa.

Leo Jumapili, tarehe 25 Aprili 2021, Mnyika kupitia ukurasa wake wa Twitter ameandika, kuwa Rais Samia amewajibu barua hiyo na sasa wanasubiri kupangiwa tarehe.

“Naomba kuwapa taarifa rasmi kuwa tarehe 20 Aprili 2021, tulipokea majibu ya barua ya Mh. Mwenyekiti, Freeman Mbowe ya kuomba kukutana na Mh. Rais Samia Suluhu Hasaa.”

“Rais amekubali kukutana kushauriana na Chadema. Tunasubiri kujulishwa tarehe ya kukutana,” amesema Mnyika

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Sabaya afutiwa kesi, ruksa kugombea uongozi

Spread the loveMwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali DPP leo Ijumaa amefuta rufaa...

Habari za Siasa

Serikali yasaka bilioni 3 kujenga daraja Mto Mpiji

Spread the loveSerikali imesema inaendelea na juhudi za kutafuta fedha kiasi cha...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kwafukuta kisa chaguzi, Lissu aibua tuhuma nzito

Spread the loveCHAGUZI za kusaka viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo...

Habari MchanganyikoTangulizi

Kimbunga “HIDAYA” chaendelea kuimarika, wananchi wapewa tahadhari

Spread the loveMAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inaendelea kutoa taarifa...

error: Content is protected !!