Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa DED Temeke, Sumbawanga wasimamishwa kazi
Habari za SiasaTangulizi

DED Temeke, Sumbawanga wasimamishwa kazi

Spread the love

 

LUSUBILO Mwakabibi, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Temeke na Nyangi Msemakweli, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga, wamesimamishwa kazi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Taarifa ya wakurugenzi hao kusimamishwa kazi imetolewa na Nteghenjwa Hosseah, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano cha Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi).

Taarifa hiyo imeeleza Ummy Mwalimu, Waziri wa Tamisemi, amewasimamisha kazi wakurugenzi hao kwa makosa mbalimbali ikiwa ni pamoja na ubadhirifu na usimamizi usioridhisha wa miradi ya maendeleo.

Waziri Ummy Mwalimu

Taarifa hiyo imefafanua, kwamba uamuzi huo umefikiwa baada ya Tamisemi kupokea malalamiko na tuhuma kutoka mbalimbali za wananchi dhidi ya viongozi hao kuhusika na mwenendo wenye mashaka.

Na kwamba, Mwakabibi anatuhumiwa kuhusika na matumizi mabaya ya madaraka, ubadhirifu na usimamizi usiofaa wa miradi ya maendeleo.

Mwakibibi amewahi kuingia kwenye mgogoro na wanahabari kwa muda sasa kwa sababu ya kukataa kutoa taarifa mbalimbali anazoulizwa na siku chache zilizopita, aliamuru kukamatwa kwa waandishi wawili kwa madai waliingia kwenye mkutano wake na wafanyabiashara bila idhini yake.

Taarifa hiyo pia imeeleza, tuhuma zinazomkabili Msemakweli ni ubadhirifu, usimamizi mbovu wa miradi ya maendeleo na uhusiano usioridhisha kati yake na madiwani, Mkuu wa Wilaya na viongozi wengine wa Wilaya na wa Mkoa wa Rukwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!