KUFUATIA tishio la Kimbunga JOBO, Ofisi ya Waziri Mkuu imeeleza kusitisha usafiri wa anga, baharini na shughuli mbalimbali kando na ndani ya Bahari ya Hindi. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).
Hata hivyo, taarifa ya Mamlaka ya Hewa Tanzania (TMA), imeeleza kwamba kadri kimbunga hicho kilivyokuwa kikielekea pwani ya Mafia, kilikuwa kinapoteza nguvu kutokana na kukumbana na upepo kinzani.
Waziri wa Nchi, Ofisi wa Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na watu wenye ulemavu, Jenister Muhagama ameelekeza Kamati za Usimamizi wa Maafa za mikoa, wilaya, kata na vijiji kuchukua tahadhara endapo athari zitatokea.
Muhagama ameagiza menejimenti za maafa ziwashauri wananchi kuhakikisha paa zao zinakuwa imara ikiwa ni pamoja na kukata matawi ya miti iliyopo karibu na nyumba, kufunga milango na madirisha muda wote.
Na kwamba, mambo mengine ambayo kamati hiyo inapaswa kuwashauri wananchi ni pamoja na kuweka akiba ya kutosha ya chakula.
Kwa upande wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), imeelekeza kusimamisha shughuli zote za baharini mpaka hapo taarifa mpya itapotolewa.
Leave a comment