Wednesday , 29 March 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko Kimbunga JOBO: Usafiri wa anga, baharini wasitishwa
Habari Mchanganyiko

Kimbunga JOBO: Usafiri wa anga, baharini wasitishwa

Spread the love

 

KUFUATIA tishio la Kimbunga JOBO, Ofisi ya Waziri Mkuu imeeleza kusitisha usafiri wa anga, baharini na shughuli mbalimbali kando na ndani ya Bahari ya Hindi. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Hata hivyo, taarifa ya Mamlaka ya Hewa Tanzania (TMA), imeeleza kwamba kadri kimbunga hicho kilivyokuwa kikielekea pwani ya Mafia, kilikuwa kinapoteza nguvu kutokana na kukumbana na upepo kinzani.

Waziri wa Nchi, Ofisi wa Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na watu wenye ulemavu, Jenister Muhagama ameelekeza Kamati za Usimamizi wa Maafa za mikoa, wilaya, kata na vijiji kuchukua tahadhara endapo athari zitatokea.

Muhagama ameagiza menejimenti za maafa ziwashauri wananchi kuhakikisha paa zao zinakuwa imara ikiwa ni pamoja na kukata matawi ya miti iliyopo karibu na nyumba, kufunga milango na madirisha muda wote.

Na kwamba, mambo mengine ambayo kamati hiyo inapaswa kuwashauri wananchi ni pamoja na kuweka akiba ya kutosha ya chakula.

Kwa upande wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), imeelekeza kusimamisha shughuli zote za baharini mpaka hapo taarifa mpya itapotolewa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Rais Samia awataka wahariri kufanya kazi bila uoga, upendeleo

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan amewataka wahariri wa vyombo...

Habari Mchanganyiko

STAMICO yasaini mkataba wa bilioni 55.2 kuchoronga miamba GGML

Spread the loveSHIRIKA la Madini la Taifa (STAMICO) limezidi kufanya vizuri katika...

Habari Mchanganyiko

NMB yatoa traksuti za Mwenge wa Uhuru Mtwara

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa traksuti kwa mkoa wa Mtwara ambako...

Habari Mchanganyiko

Yara yaja na bima ya mazao kwa wakulima

Spread the love  WAKATI serikali ikiweka mikakati mbalimbali kuimarisha sekta ya kilimo...

error: Content is protected !!