Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Kimbunga JOBO: Usafiri wa anga, baharini wasitishwa
Habari Mchanganyiko

Kimbunga JOBO: Usafiri wa anga, baharini wasitishwa

Spread the love

 

KUFUATIA tishio la Kimbunga JOBO, Ofisi ya Waziri Mkuu imeeleza kusitisha usafiri wa anga, baharini na shughuli mbalimbali kando na ndani ya Bahari ya Hindi. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Hata hivyo, taarifa ya Mamlaka ya Hewa Tanzania (TMA), imeeleza kwamba kadri kimbunga hicho kilivyokuwa kikielekea pwani ya Mafia, kilikuwa kinapoteza nguvu kutokana na kukumbana na upepo kinzani.

Waziri wa Nchi, Ofisi wa Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na watu wenye ulemavu, Jenister Muhagama ameelekeza Kamati za Usimamizi wa Maafa za mikoa, wilaya, kata na vijiji kuchukua tahadhara endapo athari zitatokea.

Muhagama ameagiza menejimenti za maafa ziwashauri wananchi kuhakikisha paa zao zinakuwa imara ikiwa ni pamoja na kukata matawi ya miti iliyopo karibu na nyumba, kufunga milango na madirisha muda wote.

Na kwamba, mambo mengine ambayo kamati hiyo inapaswa kuwashauri wananchi ni pamoja na kuweka akiba ya kutosha ya chakula.

Kwa upande wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), imeelekeza kusimamisha shughuli zote za baharini mpaka hapo taarifa mpya itapotolewa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!