Saturday , 25 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Mnyika: Rais Samia amejibu barua ya Mbowe
Habari za SiasaTangulizi

Mnyika: Rais Samia amejibu barua ya Mbowe

Rais Samia Suluhu Hassan
Spread the love

 

JOHN Mnyika, Katibu Mkuu wa Chama Kikuu cha Upinzani Tanzania- Chadema amesema, Rais wa nchi hiyo, Samia Suluhu Hassan, amekubali wito wa chama hicho, kukutana na kushauri mambo mbalimbali. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Ni baada ya Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, kuueleza ulimwengu kuwa, wamemwandikia barua Rais Samia ya kuomba kuonana naye.

Mbowe aliyasema hayo tarehe 11 Aprili 2021, alipozungumza na Watanzania kupitia vyombo vya habari, kuhusu mambo kadhaa ikiwemo kifo cha aliyekuwa Rais wa Tanzania, John Pombe Magufuli.

Hayati Magufuli, alifariki dunia tarehe 17 Machi 2021, katika Hospitali ya Mzena, Dar es Salaam na mwili wake, kuzikwa nyumbani kwao Chato mkoani Geita 26 Machi 2021.

Mara baada ya kifo hicho, Samia aliyekuwa makamu wa Rais, aliapishwa kuwa Rais kwa mujibu wa Katiba ya Tanzania.

Katika maelezo yake Mbowe aliyoyatoa, alisema, Chadema imemwandikia barua Rais Samia ya kuomba kuona naye ili wazungumze masuala mbalimbali yenye manufaa kwa Taifa.

Leo Jumapili, tarehe 25 Aprili 2021, Mnyika kupitia ukurasa wake wa Twitter ameandika, kuwa Rais Samia amewajibu barua hiyo na sasa wanasubiri kupangiwa tarehe.

“Naomba kuwapa taarifa rasmi kuwa tarehe 20 Aprili 2021, tulipokea majibu ya barua ya Mh. Mwenyekiti, Freeman Mbowe ya kuomba kukutana na Mh. Rais Samia Suluhu Hasaa.”

“Rais amekubali kukutana kushauriana na Chadema. Tunasubiri kujulishwa tarehe ya kukutana,” amesema Mnyika

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia aagiza iundwe kamati ya pamoja ya Mawaziri mradi wa BBT

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amewaagiza mawaziri kuunda kamati...

Habari za Siasa

Rais Samia apangua makatibu tawala mikoa, ateua Kamishna DCEA

Spread the loveALIYEKUWA Kamishna wa Mamlaka ya Kudhibiti Dawa za Kulevya, Gerald...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

M/kiti bodi ya wadhamini Chadema afariki dunia

Spread the loveMWENYEKITI wa Bodi ya Wadhamini ya Chama cha Demokrasia na...

Habari za Siasa

Zitto: Nikifa Ado atavaa viatu vyangu

Spread the love  KIONGOZI Mkuu wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe...

error: Content is protected !!