Saturday , 4 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa ‘Kikwete, Kinana, Ndugai wamewakosea nini?’
Habari za SiasaTangulizi

‘Kikwete, Kinana, Ndugai wamewakosea nini?’

Spread the love

 

TABIA ya kusemwa vibaya Rais Mstaafu, Jakaya Kikwete; Spika wa Bunge, Job Ndugai; Abdulrahman Kinana na Nape Nnauye, Mbunge wa Mtama kumemkera Deo Sanga, Mbunge wa Makambako (CCM). Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Akizungumza bungeni leo tarehe 21 Aprili 2021, wakati wa mjadala wa Bajeti ya Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) kwa mwaka 2021/2022, Sanga amesema, tabia ya kuwasema wastaafu na wabunge hao ikomeshwe na kwamba, ikiachwa itasababisha sintofahamu.

Amesema, kwenye mitandao ya kijamii, viongozi hao wamekuwa wakinangwa huku mamlaka husika vikiangalia, amesisitiza kwa jambo hilo halipaswi kuachwa liendelee.

“Nani atafuata mheshimiwa spika? Hii ni hatari. Ni lazima tukemee kwa jambo ambalo linaweza kutugombanisha Watanzania, tukiliacha likaendelea, kesho kutwa hatujui atawekwa nani,” amesema.

Sanga amesema, Rais Kikwete amefanya kazi kubwa kwenye utawala wake, ametaka wanaomsema vibaya wamwanche apumzike huku akibainisha kazi kubwa iliyofanywa na Nape pia Kinana, Katibu Mkuu wa CCM wa zamani mwaka 2013-2015, ilikuwa ya kutukuka.

“Mheshimiwa Kikwete akapumzike, amefanya kazi yake vizuri, Kinana akapumzike. Nape wewe ni shahidi 2013 – 2015 wakati wa uchaguzi, Nape na Kinana walizunguka miaka mitatu kutafuta kura za CCM,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Sabaya afutiwa kesi, ruksa kugombea uongozi

Spread the loveMwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali DPP leo Ijumaa amefuta rufaa...

Habari za Siasa

Serikali yasaka bilioni 3 kujenga daraja Mto Mpiji

Spread the loveSerikali imesema inaendelea na juhudi za kutafuta fedha kiasi cha...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kwafukuta kisa chaguzi, Lissu aibua tuhuma nzito

Spread the loveCHAGUZI za kusaka viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo...

Habari MchanganyikoTangulizi

Kimbunga “HIDAYA” chaendelea kuimarika, wananchi wapewa tahadhari

Spread the loveMAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inaendelea kutoa taarifa...

error: Content is protected !!