Sunday , 19 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia kupangua makatibu wakuu
Habari za Siasa

Rais Samia kupangua makatibu wakuu

Rais Samia Suluhu Hassan
Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amesema, atafanya mabadiliko ya makatibu wakuu wa wizara mbalimbali hivi karibuni. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Amedokeza hilo leo Alhamisi tarehe 1 Aprili 2021, Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma, mara baada ya kumaliza kuwaapisha mawaziri, naibu mawaziri na katibu mkuu kiongozi waliowateua jana Jumatano.

Akianza kuzungumza kwa kuwasalimia viongozi mbalimbali waliohudhulia hafla hiyo, Rais Samia aliuliza makatibu wakuu mpo, heloooo…kisha wakasimama kumsalimia naye akasema mmetulia ninyi “siyo leo lakini nakuja.”

Mara baada ya kumaliza hotuba yake fupi, Rais Samia akizungumzia sikukuu ya Pasaka akisema kuanzia kesho Ijumaa hadi Jumatatu ni sikuu “tutakutana hapa Jumanne” kushuhudia wengine wakiapishwa.

Hata hivyo, Rais Samia hakusema hasa hiyo Jumanne, watakaoapishwa watakuwa makatibu wakuu au wengine, kama wakuu wa mikoa, wilaya au makatibu tawala wa mikoa.

Rais Samia amewaonya wateule wake, watakaokuwa wakipandisha mabega akisema “nitakuwa na kipimo cha mabega, nikiona mtu anapandisha mabega nitaona huyu si mtumishi wa wananchi.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Wakili Mwabukusi anusurika kufungiwa, asema hatarudi nyuma

Spread the loveWAKILI Boniface Mwabukusi amesema kuwa hatorudi nyuma kuwatetea Watanzania na...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

RC Chongolo atangaza ‘vita’ kwa wanaovusha wageni kinyemela

Spread the loveKATIKA kulinda usalama wa nchi kupitia mpaka wa Songwe, Mkuu...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

RUWASA yachongewa, yateketeza mamilioni kwa maji yenye magadi

Spread the loveSAKATA la ukosefu wa maji wilayani Momba mkoani Songwe limezidi...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Lissu akabidhiwa gari lake, aomba msaada wa matengenezo

Spread the loveMakamu Mwenyekiti wa Chadema Bara, Tundu Lissu leo Ijumaa amekabidhiwa...

error: Content is protected !!